Unabii 20

Jihadharini na Hofu ya Pigo Mpya la Damu Nyeusi Inayochemka Ijayo!

Mchungaji Mtume Sherrie Elijah (Elisheva Sherrie Eliyahu) Mei 25, 1998

Haya maneno yanatoka kwenye Unabii wa 105, YAHUVEH Alisema yaongezwe kwenye Unabii zote kutoka sasa: Nilikuonya kitambo Elisabeth [Elisheva], kutoita Huduma hii kwa jina la mwanamume au mwanamke. Hata kabla kuwepo na Huduma, Niliiweka ndani ya roho yako. Kwa kuwa hakuna lolote lililofanyika kwa mikono yako. Hakuna lolote lililotoka kwenye kinywa chako. Ilitoka kwenye Kinywa cha YAHUVEH Aliyeizalisha. Ilitoka kwenye Kinywa cha YAHUSHUA, MASHIACH wako Aliyeizalisha. Ilitoka kwenye Kinywa cha RUACH HA KODESH, IMMAYAH wako Aliyeizalisha. Kama ingekuwa tu kwa mkono wako, ingekuwa imefeli kitambo. Ni kwa UPEPO WA SHKHINYAH GLORY unaovuma kote duniani, UPEPO TAKATIFU WA UAMSHO. Sio kwa pumzi yako, au ingekuwa imefeli. (Isaya 42:8)

Katika mwezi wa Julai 2010, MUNGU YAHUVEH pia Alisema kuongezwe yafuatayo mbele ya Unabii zote:

2 Mambo ya Nyakati 36:16, “Lakini waliwadhihaki Wajumbe wa MUNGU, na kuyadharau Maneno YAKE, na kuwacheka Manabii WAKE, hata ilipozidi Ghadhabu ya BWANA juu ya Watu WAKE, hata kusiwe na kuponya.”

* * * * * * *

Maoni kwa Unabii huu

YAHUSHUA Alizungumza nami kama ninavyozungumza nanyi sasa, na maneno yaleyale. Hamna chochote Atakachoruhusu ndani ya maisha yetu tena ambacho kitaleta aibu kwa kile ambacho Ametuita sote kufanya na kufanikisha katika Jina Lake. YAHUSHUA mwenyewe hatakuwa tu mwana kondoo lakini Simba wa Yuda Atakayerarua hicho kitu cha aibu au mtu huyo kutoka maishani mwetu kutuweka sisi watakatifu mbele Zake. Kwa kuwa ni huduma ngapi zilizoanguka kwa sababu aibu na dhambi na kufungwa nira na wasioamini imeingia na mengine zaidi!

Sijapoteza chochote. Hamjapoteza chochote kwa kuwa hatukuwahi kuwa nayo kutoka hapo mwanzoni. Ilikuwa uongo wa shetani. Kama tumefungwa nira na wasioamini na jina lao halipatikani kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-kondoo na umetoa maisha yako kwake YAHUSHUA MASIHI na unamtumikia na kumweka kwanza na kuzungumza kama mdomo Wake, kwa uhakika Mungu yuyo huyo unayemtumikia ni Mungu mwenye wivu na YEYE hatatugawa na shetani kwa njia yoyote, muundo au umbo. Baba YAHUVEH mwenyewe kwa uzuri wako Atakutenga kutoka kwa yale ambayo sio takatifu na kukubalika mbele ya RUACH ha KODESH!

Atayafanya haya kwa upesi sasa kwa kuwa Terrah umekoroga upako ndani yangu kupitia unabii huu na majeraha niliyoyapata yamenifanya niwe na nguvu mara nyingine kama yatakavyotufanya sote. Ndani ya mwili wetu tunahisi tumegongwa na kukanyagwa na kutemewa mate, lakini lazima tuendelee kuinuka katika jina la YAHUSHUA na sio mwili wetu kuinuka lakini Roho ndani yetu, ndiposa itakuwa ni shetani aliyegongwa, kukanyagwa chini ya miguu yetu katika jina la YAHUSHUA!

* * * * * * *

Hivi ndivyo Asemavyo YAHUVEH; Katika nyakati zilizopita Nilipambana na watoto WANGU waliofungwa nira na wasioamini, watumishi WANGU, wale wanoitwa kwa Jina LANGU waliojifunga nira na watoto wa shetani kupitia ndoa, urafiki, ushirikiano, mashirika, kanisa na mifano nyingine. Kwa ajili yenu Nimepambana nanyi kwa utulivu na kuvumilia. Nilingoja Watoto WANGU kutambua ambapo RUACH ha KODESH haheshimiwi, wala kupendwa wala kukaribishwa hata kama ni ndoa, familia, urafiki, shirika au chochote kile kisicho cha KWANGU, wewe kwa kweli sio mmoja wao na hawajawahi kuwa moja nawe.

Wengi wamefanya chaguo mbaya na alafu ni MIMI Ninayelaumiwa. Kwa kuwa wanapojeruhiwa na kuja kwa Baba na kusema, “Baba angalia majeraha YANGU ya Damu, angalia kile ninaowapenda walichonifanyia, wale niliowaamini, wale niliojifunga nira nao. Baba, mbona uliruhusu haya yafanyike? Je, haujali?” O watoto WANGU, ndio, ndio tena Ninasema kwenu nyinyi Ninajali na Nitayasema haya kama Nimefungua Mikono YANGU ili mkimbie pale ndani na kupanda kwenye paja la Baba Mungu wenu YAHUVEH na Ninawakumbatia mikononi MWANGU, kuwaruhusu kulia machozi machungu. Kwa kuwa mmekuwa mkiyaweka ndani kwa muda mrefu na zinapoachiliwa, mnapotambua kuwa sio MIMI Niliowaweka pamoja, Niliowaunganisha na uasi.

Ni wewe mwenyewe uliojifunga nira na dhambi ya dunia hii kwa kuwa ukawa kama yule aliye moja na dhambi ulipochagua kuoa bila kuniuliza MIMI kama mtu huyo alikuwa mchumba sawa kwako. Kama huyu ndiye yule aliyekadiriwa kabla ya kuumbwa kwa dunia, kuwa wako? Wakati mlipojifunga nira na dhambi, mlipokuwa viongozi wa wapagani wanaochagua kubaki wapagani, mlifunga macho yenu kwa hivyo Baba yenu YAHUVEH imembidi kufungua macho yenu kwa nguvu Akiwalazimisha kuona yale ambayo hamkuona hapo awali.

Mmejifunga nira na shetani kwa kuwa watoto wenu wanapopotea njia na kunikataa MIMI na ‘walipofunzwa ni njia gani wanafaa kuenda’, Nilisema, “watakapokuwa wakubwa hawataondoka pale” na bado mnaona watoto wenu mliowalea kwa njia za Mungu na mnashangaa kinachoendelea? Ni kwa sababu mliruhusu watoto wenu kujifunga nira na wasioamini kupitia televisheni wanayoitazama, muziki wanayosikiliza pia, michezo wanayocheza, Marafiki wanaowaita wenzao na shule ambazo wanapoenda.

Mnaruhusu wapagani kuwafunza watoto wenu ili kupata masomo ya dunia ya bure, alafu mnakuja KWANGU na kutaja maandiko, “Funza mtoto wako katika njia ifaayo na watakapokuwa wakubwa hawataiacha,” na kumbe mliporuhusu haya mmefeli kwa kuwafunza. Mlipoacha kusoma Bibilia na mkawaamini kusema maombi yao wenyewe, mnapooa na hamniulizi MIMI ni nani aliyefaa kuwa Baba au Mama uliyejifunga nira naye, kukuja juu yenu.

Mnaposikia sauti YANGU ikisema, “Jitenge,” huruma YANGU imerushwa kwenye uso WANGU na tena ni lazima mjitenge kutoka kwa yale ambayo yanataka kuiba nafsi zenu! Kama haya hayatafanywa kwa hiari kama msimamo wa Utakatifu basi Nitafanya yale Niliyoyataja hapa na katika njia zingine zaidi, itakuwa mkono wa YAHUVEH utakaowaondoa kwa nguvu kutoka kwa utumwa wa maadui mlipofungwa nira na wasioamini. Sitagawa tena Watumishi, Watoto na Bibi Arusi WANGU na shetani! Kwa kuwa kama Umesikia sauti YANGU ikisema, “Acha huyu mtenda dhambi” na mmefanya mioyo yenu kuwa ngumu na kusema, “lakini huyu ni rafiki, huyu ni bwana, huyu ni bibi, huyu ni mtoto, hii ni kanisa langu, hii ni kazi yangu,” na msiponitii Ninahuzunishwa kwa yale lazima Nifanye.

Hii ndio nchi inayosema kuwa kuavya mimba ni halali na sasa watu wanaachwa njaa hadi kufa inavyokuwa gharama kuu zaidi kuwashughulikia wagonjwa na euthanasia itaenea zaidi kushinda hapo awali. Hivi karibuni amri zitapitishwa zikiwalazimisha madaktari kuua au cheti chao cha kazi kitachukuliwa. Madaktari, ni heri kwenu nyinyi mkatae kuliko hasira ZANGU kuwaangukia kwa sababu ya kuchukua maisha ambayo haukuwa na haki ya kuichukua. MIMI pekee Nina haki hiyo kwa kuwa Ninawatabiria sasa, kwa wakati huu ni wale ambao wana magonjwa mabaya au wale walio walemavu au wazee lakini kupitia chombo hiki Ninasema kuwa hivi karibuni itakuwa wale watakaosema ni wazimu watakaouwawa.

Dkt. Kevorkian sio binadamu, anafanana binadamu lakini wale na macho ya kuona na masikio ya kusikia wanaona pepo inayokejeli kwa macho yake na umbo la kichwa chake hata inafanana na fuvu. Kwa kweli yeye ni Dkt. Kifo na pepo ya kifo na kujiua ameileta kule Marekani na duniani na kwa wale Niliowapa upako wa kuokoa maisha kupitia Mikono ya madaktari na wale walio na maarifa ya kuokoa maisha watalazimishwa kuchukua maisha.

Hakuna yeyote aliye na haki ya kumaliza maisha ila tu yule Anayetupa maisha na MIMI, YAHUVEH, Ndiye pekee Anayewapa maisha na ana mamlaka ya kumaliza maisha. Kama amri ZANGU hazijakadiri haya, msichukue dhambi hii juu yenu, kwa kuwa sio tu mwili tu uliofariki lakini ni nafsi ambayo inatumwa Mbinguni au jehanamu. Kwa wale wanaosema, “Aaah, afadhali walienda Mbinguni” lakini je, walimaliza Nilichowaumba kufanya? Je, misheni yao hapa duniani ilikwisha, wajuaje?

Watoto, watoto WANGU Ninaowathamini, je, kuna kitu kingine kilicho cha thamani kushinda mtoto, iwe ni binadamu au mnyama? Nilichukua wakati kumwaga uzuri na unyofu ndani ya watoto na hata hivyo wanauwawa. Watoto WANGU Ninaowathamini wanauwawa kama bado walipo ndani ya tumbo za mama zao. Sasa mgeni anapofanya haya, dunia hushtuka kwa hofu wakati mauji yanapotendeka na mtoto anakatwa kutoka kwa tumbo la mamake katika matendo ya kishetani na kwa kweli watoto WANGU hawauliwi na wageni wa kishetani, hapana, ni kitu kinachosikitisha zaidi. Watoto WANGU wanauwawa kwa mama zao wenyewe.

Wale ambao Ninachukua wakati wa kuweka maziwa kwenye matiti zao ili waweze kuwalisha watoto wao na kuwatunza wachanga. Wale ambao Ninaweka upendo wa mama ndani yao kuwalinda wale bado hawajazaliwa na ni wangapi kati ya hawa ambao watoto hawa wanyofu wangeita Mama wanasalitiwa na wale wale Niliowaamuru “zaeni na mkaongezeke.” Hakuna yeyote anayewalazimisha hawa akina mama kuwaua watoto wao; wanayafanya haya na habithi na kupanga. Wanafanya haya licha ya MIMI kuwaweka mashujaa WANGU mbele ya kliniki za kuavya mimba, wakitoa ushuhuda wa upendo WANGU. Wanafanya haya kama kitendo cha uasi dhidi ya Mungu wa Viumbe vyote na tena Ninawapa unabii mwingine wa kushtua kupitia huyu Ninayezungumza kupitia kwake. Dunia itamwita yeye mjinga mpaka Ninachozungumza kitakapofanyika na itakuwa ni nyinyi mnaoua watoto WANGU katika vyumba vyenu vya kuavya mimba, nyinyi mnaouza vipande vya miili ya watoto na kutengeneza vipodozi na kuvitumia kwa sababu zingine chafu.

Nyinyi wamama mnaoruhusu miili ya watoto wenu kutozikwa lakini kutupwa kwenye pipa. Nyinyi mnaovuka barabara au kujificha kutoka kwa Watoto WANGU, wanaozungumza maneno YANGU wakiwaomba msifanye kitendo hiki cha unyama. Shetani anaogopa nguvu ya maombi sana mpaka yeye hutumia watu wake kujitoa kupiga bomu hizi kliniki kuwaua madaktari ili amri zitengenezwe zinazosema kuwa watumishi WANGU hawaruhusiwi kuwa karibu na wale ambao wako tayari kufanya kitendo hiki cha mauaji kwa watoto waliowaamini mama zao na wanaoniamini MIMI kuwalinda kutoka kwa maovu haya.

O ni mara ngapi Nimejuta kuwapa chaguo bure, lakini Nilijua ni nini kitakachofanyika kwa kuwa Mungu mnayemtumikia ni maarifa, au sivyo? Ninawatabiria haya kupitia huyu handmaiden Sherrie Elijah [Elisheva Sherrie Eliyahu], kutakuwa na mashimo makubwa yatakayofunguka chini ya kliniki za kuavya mimba kote duniani na itakapofanyika mtajua kuwa ni Mungu wa Viumbe na sio mkono wa binadamu iliyofanya haya.

Watu wote katika kliniki hizi wanaoshiriki katika tunda hili ovu la mauaji watakufa na dunia itafunguka na mtetemeko wa ardhi kuu utalia na klinilki za kuavya mimba zitaanguka ndani kwenye ardhi na tena ardhi itawafunika juu. Kliniki hizo zote zitashuka hadi kwenye matumbo ya jehanamu katika njia ambayo haijawahi kufanywa tangu nyakati za kale. Dunia itatingiza vichwa vyao kwa kuwa watalazimishwa kukubali kuwa hii haikuwa bomu kutoka dunia lakini ni bomu kutoka Mbinguni na Mungu wa Viumbe vyote, Mungu Mkuu YAHUVEH Atayafanya vitu hivi na zaidi kwa kuwa ardhi hii imejawa na maovu na ponografia zenu na usherati wenu na kila aina ya maovu.

Nitafanya ishara na mishangao kuonyesha ghadhabu YANGU kwa yeyote atakayethubutu kuonyesha pepo hii ya sodoma na gomora kwa uso WANGU! Stesheni za televisheni zilizopata faida kutoka kwa ponografia na aina zote za kunikejeli MIMI na stesheni za redio jihadharini, kwa kuwa mmejenga mnara wa Babeli na mnafikiria kuwa hakuna yeyote anayeweza kuugonga lakini MIMI Nitafanya hivyo. Mungu wa Viumbe vyote Atawaonyesha vile minara yenu na vipokeaji vyenu ni vidhaifu.

Ushoga ambao ulikuwa kwa uchache sasa utaiona ukiwekwa mbele ya watoto WANGU Watakatifu na watoto wao na hata watoto wa wapagani wakisema, “Hii ni njia nyingine ya kuishi bora tu ni upendo, tunaumiza nani?” Nitawaambia ni nani mliyoumiza, mmeweka ghadhabu ZANGU juu yenu, Mungu Aliyekadiri na kuwapa Amri Kumi kwa Musa na kukataa vitu kama hivi na hata kuamuru mwanamke atakayelala na mwanamke mwingine, au mwanamume atakayelala na mwanamume mwingine, KUUWAWA ili maovu haya yasienee.

Wale ambao hufanya ngono na wanyama walipaswa KUUWAWA! O lakini sasa nchi hii mbovu inafanya haya yote yaliyo maovu mbele ya uso WANGU. Fanya unachotaka angalau tu inakufanya ujisikie vizuri ndio kanuni yao. Ponografia, ushoga, uzinzi ni mtego wa shetani kwa kuwa inaleta hamu kubwa ya uchafu na usherati na hujaribu kufanya zaidi ya kitendo cha mwisho. Shetani anatafuta kuchafua binadamu zaidi kila wakati kupitia pepo hizi. Shetani hapendi YEYOTE, hawapendi hata wale wanaomuabudu. Anawavuta kupitia dhambi hizi na ndio hata anawatuza raha za dhambi, lakini mwishowe watapoteza nafsi zao wasipotubu na wasipoacha hizi dhambi, itaisha kwa uharibifu milele na mmeonywa!

Sasa tena Ninawatabiria kupitia huyu handmaiden WANGU. Itakuwa vizuri kwenu kuomba masikio yasikie sauti YANGU na macho kuona yale yatakayokuja hivi karibuni. Mtaona ugonjwa mpya utakaokuwa mbaya zaidi kushinda ukimwi kwa kuwa Nimezungumza hapo awali lakini sio kwa sauti ya juu. Sasa, lazima mmwaonye wote wanaosikia ujumbe huu kwa kuwa wale walio na kijiko cha fedha na wanawalisha Watoto WANGU wakisema kuwa hakuna chochote kibaya na vitu vilivyotajwa hapo juu. Kuna pigo mpya linalokuja ambalo halitaguza yeyote aliye mtakatifu na asiyefanya vitu hivi, kwa hivyo msiwe na hofu. Litakuwa pigo linaloeenea kwa njia ya ngono na dunia hii iliyo na dhambi imepatikana katika mtego WANGU.

Nikijua maovu ya hamu yao ya ngono ambayo haiwezi kutoshelezwa kwa hivyo Mungu wa Viumbe vyote, MIMI, YAHUVEH, Niliruhusu dawa hii kutengenezwa. Dawa hii ya ngono binadamu atalipa gharama kwa ajili yake na watakuwa na nguvu ya ngono ya kuwatafuta wapenzi wengine. Ile tamaa ambayo watakuwa nayo kwa wengine hata kama ni kwa wale walio hisia sawa au la kama wao wameolewa au la, kama tembe hizi au sindano itagharamiwa na mshahara wa wiki mzima, kwa sasa inaanza na bei moja lakini watakapokuwa wamezoea dawa hizi na hawawezi tena kuwa kama walivyokuwa kwa ngono kama tamaa hii inashughukuliwa, watalipa mshahara wao mzima kupata tembe hii.

Kwa kuwa shetani ameiweka hii tamaa ndani ya hawa wanaume ni kama moto ya jehanamu. Haiwezi kuzimwa. Hawataweza kutoshelezwa na ngono. Mabwana watawaacha bibi zao na mabibi watawaacha bwana zao na watoto watakimbilia haya, sanasana vijana. Kama mnafikiria kuwa watoto ni waasi sasa, ngojeni hadi maovu haya yanayosifiwa kama dawa ya muujiza ithibitishwe kuwa laana kutoka kwa shetani, Niliruhusu ije juu ya taifa hili na ndio, dunia. Deni kubwa zitakuja, kwa kuwa hata kadi za mkopo zitaonyesha tamaa ya dawa hii.

Wakati dawa hii itasimamishwa kwa sababu yeyote, kutakuwa na hamu ya ngono na kutokuwa na njia ya kuendelea bila dawa hii, kwa hivyo uhalifu zitafanyika kwa sababu ya dawa hii ili watu waweze kuinunua. Tena Watoto WANGU hawana chochote cha kuogopa kwa kuwa Ninawaamuru sasa hivi, msijihusishe na haya kabisa. Nimekadiri kuwa ngono ni takatifu inapofanyika na mtu ambaye amefungwa nira na anayeamini katika ndoa, hapa ndipo Baraka zenu zilipo. Lakini kimbieni jaribio hili kwa kuwa kutakuwa na matangazo ambazo zitawaambiwa kuwa dawa hii ni sawa, Nimetabiri jinsi tamaa hii itakavyokuwa, ni nyumba ngapi zitapotea, ndoa ngapi zitakazoharibika na ndio hata watoto WANGU wengine wataniacha MIMI kwa kuwa pepo ya usherati ipo ndani ya dawa hii.

Handmaiden huyu ndiye wa kwanza Niliyemchagua kuzungumza kwa ujasiri na bila hofu ya matokeo. Sherrie Elijah [Elisheva Sherrie Eliyahu] hana maarifa yoyote kuhusu dawa hii ila tu yale Ninayozungumza sasa. Niliruhusu maovu haya kuja ili Watoto WANGU tena waone kuwa MIMI sio Mungu wa kukejeliwa virahisi. Nitawapa dunia hii yenye dhambi chaguo la kuchagua lakini itakuja na gharama. Sasa laana nyingine itakuja juu ya dawa hii muujiza ya ngono, mungu mpya wa dunia hii yenye dhambi. Kwa kuwa kutakuwa na ukosefu wa dawa hii, hivyo ndivyo watakavyosema, na itakuwa vigumu sana kuipata, alafu mtaona mauaji juu ya dawa hii. Lakini mwisho na laana kuu ya yote ni, itakapoingia kwenye mikono ya mashoga na waingie katika hizi uhusiano chafu. Ninawatabiria sasa pigo Nililiozungumzia hapo awali ambayo itakuwa na dalili mbaya zaidi kushinda ukimwi, iliyo na makali na uchungu na HAKUNA YEYOTE ambaye anachukua dawa hii baada ya onyo LANGU ataiepuka.

PIGO LA DAMU NYEUSI INAYOCHEMKA!!!

Kwa kuwa kutakuwa na laana kwenye damu na homa kali, njaa na kutoweza kula. Damu itamwagika kutoka kwa mdomo na itakuwa ni kama damu imebadilika kuwa nyeusi itamwagika kutoka kwa sehemu ya miili iliyo wazi. Wanaume na wanawake wataipata kutoka kwa mkutano MMOJA tu wa ngono na yeyote aliye nayo, Ninasema tena, kama huyu ni nabii WANGU anayezungumza na roho yako itakuwa tayari imepata ushuhuda kwa haya sasa, MOJA, mmeniskia MIMI, mkutano MMOJA, Ninarudia tena, ndio itakayochukua na pigo hili litakuja juu yao kwa njia ile ile kama vile dawa hii muujiza ya ngono iliyokuja juu ya dunia hii kwa ghafla na kwa haraka HAKUTAKUWA NA TIBA Ninarudia tena hata baada ya wao kutubu wakiwa wanakufa vitandani mwao.

Nimeponya ukimwi kwa hata wale wasio na hatia wamepata kuwa usambazaji wa damu imechafuliwa na Nimewaponya wengine, ingawa ugonjwa huu ulitoka kwa dhambi ya ngono na wanyama, tumbili. Binadamu akikejeli lile Nilikusudia kuwa takatifu, wakifanya ngono na tumbili. Je, ni mshangao kuwa mwanamume kufanya mapenzi na mwanamume, kitendo kingine kichafu, chukizo katika macho YANGU iliisambaza kupitia ushoga? Lakini ugonjwa huu husafiri kwenye damu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa pigo hili lipya, kwa kuwa DAMU YA YAHUSHUA MASIHI ilikataliwa na kuna wokovu katika Damu hiyo, kwa hivyo mbona Nisilaani damu ya wale wanaonikejeli MIMI Nilivyowapa Mwana WANGU YAHUSHUA kuwa Dhabihu yao ya Damu, Nikijua kuwa ni wachache tu watakaoshukuru.

Nimeponya UKIMWI lakini pigo hili la nyakati hizi za mwisho, hakuna yeyote atakayeponywa. Ingawa watatubu na kukubali damu ya wokovu ya YAHUSHUA wataokolewa lakini bado watakufa kwa kuwa watavuna yale waliyopanda. Ingawa mwili utakufa, nafsi itaenda Mbinguni kama kweli waliacha dhambi hii, kumpenda na kumtumikia YAHUSHUA, wakijua kuwa Alilipa gharama ya dhambi zao na kuwaosha na Damu YAKE inayookoa.

Wale watakaofanya haya, tena, watakufa lakini nafsi zao zitaokolewa na mkitaka kujua kama kwa kweli wametubu mtawaona wale walio na Pigo hili la Damu Nyeusi Inayochemka wakinikiri MIMI na kuwaonya wengine kuachana na dhambi hii ya ngono na kuishi kwa maovu. Lakini hakuna yeyote, Ninarudia, na haya ni mapya tena kwa kuwa MIMI huwa sijirudii katika unabii kama sasa lakini muwe makini Ninapofanya haya, kwa kuwa hii ni njia mpya pia Ninayotabiri siku hii. HAKUNA YEYOTE ATAKAYEPONYWA! Hili ni pigo la nyakati za mwisho mlilolisikia. Hapa ndipo wanaume na wanawake watakapotaka kufa na hata kujaribu kujiua wao wenyewe.

Euthanasia itakuwa kama hali ya kawaida na makaburi haitataka kuyazika miili hii. Lakini kuchoma maiti itakuwa njia mbadala. Laana ya uharibifu huu itabebwa kwenye damu. Kwa kuwa walivyokataa utakatifu na wakarudi kwenye maovu, wakipitisha amri ambapo ushoga ni halali, zikihamasisha yale ambayo yalikuwa kwa uchache na sasa pepo ya ushoga ipo kila mahali.

Ugonjwa huu hautakuwa na heshima kwa wapagani, hata kama wao ni matajiri au fukara, hata Ikulu itaguswa na pigo hili. Mtakapoona dalili hizi kumbukeni katika siku hii ilitabiriwa 5-4-98 (Mei 4, 1998) na ole kwa Watoto WANGU wowote wanaofikiria kuwa wanaweza kuchukua dawa hii na Nitaelewa. HAPANA, mtavuna mlichopanda kwa kuwa hii sio Baraka iliyotumwa duniani lakini ni laana. Sasa zungumza Nilichosema.

Wale watakaokejeli ndio watakaoipata kwanza. Wale watakaokasirikia handmaiden WANGU kwa kuzungumza na kuonya kwa jumbe ZANGU ndio watakaoipata kwanza. Wale watakaoasi dhidi YANGU na kusema MUNGU wa upendo hatafanya haya wataipata kwanza kwa kuwa Niliamuru ngono kuwa takatifu. Huduma na wahudumu waliozungumza maneno YANGU hapo awali wanaanguka na wameanguka na wataendelea kuanguka. Ngono ni ya wale waliounganishwa pamoja katika Ndoa takatifu ili roho hizo mbili ziwe moja. Nitabariki Niliyoweka pamoja.

Nyinyi ambao mpo katika ndoa zisizo takatifu, ambazo sijawapa njia ya kutoka bado na mmelazimishwa kukaa kwenye ndoa hizi, lakini ni kwa msimu tu, Nilisema mtalindwa kutoka kwa pigo hili, hiyo ndiyo Nilimaanisha. Kwa kuwa shetani atataka ufanye kazi yako kama bibi au bwana na kwa sababu mwenzako uliye naye, sijawatenga bado, atataka kujaribu na kumwaga pigo hili juu yako kwa kuwa Nimesema kuwa hakuna tiba na itachukua tu mara moja, na utajuaje kama mwenzako anachukua dawa hii ya ngono?

Lakini sasa Ninazungumza kwenu nyinyi mlio katika ndoa na wapagani: msiwe na hofu kwa kuwa Nitawalinda. Hii tu ndio kesi ya pekee kwa laana zilizotajwa pale juu kwa kuwa si Nilisema Nitawalinda wale ambao ni WANGU na hamna mamlaka yoyote juu ya kile bwana yako au bibi yako mpagani anachofanya. Au, kama utabakwa na mtu ambaye ana hii laana, Nitawalinda; pigo hili halitakuja karibu nanyi. Someni Neno LANGU, simameni juu yake na pia mjue jinsi Ninavyowapenda, laana hii si ya Watoto WANGU.

Ngono itakuwa mungu ya wapagani na ishakuwa lakini si wenu. Na mjue haya; hamtakuwa katika ndoa hizi kamwe. Nitatoa njia ya kuepuka, wengi watakuwa wajane na bwana ataona bibi yake akifa mbele ya macho yake. Talaka huwaweka Watoto WANGU kwenye utumwa zaidi, lakini wakiamua kukupea talaka, waache waende, Nitawashughulikia kwa njia msizozijua. Nikiamua, Nitakuletea mchumba Mtakatifu ikitegemea na mapenzi YANGU ni yapi kuhusu maisha yako, kila mmoja ni tofauti. Kwa kuwa muda ni mfupi sana. Kwa kumaliza, jueni haya na kumbukeni kuwa pigo hili sio kwa Watoto WANGU. Mtalindwa ilhali tu mtatembea kando YANGU. Msinikane MIMI kwa mungu wa dunia hii.

Msiguse dawa hii inayoitwa muujiza ya ngono! Itakuwa muujiza lakini muujiza utakuja kwa mfano wa Mwokozi mpendwa Atakayelinda yote ambayo ni YAKE wakati pigo hili na tamaa itakuwa inaangamiza dunia hii. Pigo ambalo ni hukumu ya kutotii. Mambo ya walawi 26:25, Hesabu 14:12, Kumbukumbu la Torati 28:21, Yeremia 14:12, Yeremia 27:13, Ezekieli 5:12, Ezekieli 6:11, Ezekieli 7:15, Mathayo 24:7, Luka 21:11

Someni haya: Mungu wa Wokovu, YAHUSHUA MASIHI, MASIHI wenu, Amezungumza siku hii kupitia huyu handmaiden, sio maneno yake kwa kuwa maneno yake bila Jina LANGU na upako wa RUACH ha KODESH haiwezi kumshtua mbwa. Lakini Maneno YANGU yaliyozungumza dunia hii kwa kuwepo na Mungu Mwenyezi YAHUVEH yule yule Anayezungumza kwa wale wanaosikia sauti YANGU, Amezungumza siku hii. Kwa hasira Ninaziita laana hizi. Kuna Baraka kwa wale wanaotii na laana kwa wale wanaototii. Waonye enyi manabii WANGU. Zungumza kwa sauti ya juu ili hawatasema kuwa sikuwaonya!

Luka 21:25-36, Luka 21:26. Jueni kuwa neno LANGU halitanirudia MIMI tupu. Someni maandiko na myafikirie yote. Ya mwisho ambayo Nitafanya mtumishi WANGU awakumbushe ni nyoyo za bindamu zikiwafeli kwa sababu ya hofu na kwa kutazama yote ambayo yanakuja hapa duniani, kwa kuwa nguvu za Mbinguni zitatingizwa; Luka 21:27, na wataona Mwana wa MUNGU Akija kwenye wingu la Utukufu. Na wakati vitu hivi vitakapoanza kufanyika, tazameni, nyoosheeni vichwa vyenu na mjue kuwa ukombozi wenu unakaribia.

(Yeremia:14:10-18) Hivi Ndivyo Asemavyo YAHUVEH kwa watu hawa. Nyinyi mmependa kutangatanga. Hawajazuia miguu yao, kwa hivyo YAHUVEH hawakubali. YEYE Atakumbuka maovu yao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.

Msiniulize MIMI tena kuwabariki watu hawa, msiwaombe tena. Wanapofunga, Nitawapuuza. Watakaponiletea MIMI sadaka na dhabihu, sitazikubali. Kile Nitakachowapa kama malipo ni vita, njaa, na magonjwa. Alafu Nikasema ah, Mungu Mwenyezi YAHUVEH, ndio hawa manabii, waambie, nyinyi hamtaona upanga wala hamtaona njaa, lakini Nitawapa amani katika mahali hapa. Alafu YAHUVEH Akaniambia, “unabii wa nabii upo ndani ya Jina LANGU. Sikuwatuma, wala sijawaamuru, wala sijazungumza nao.”

Kwa hivyo, hivi ndivyo Asemavyo YAHUVEH kuhusu hawa manabii wanaotabiri vitu katika Jina LANGU, wanaosema vita havitakuja au njaa, “Kwa vita na njaa, wao wenyewe watakufa na watu ambao waliowatabiria watarushwa kwenye mitaa ya Yerusalemu, waathiriwa wa njaa na vita. Hakutakuwa na yeyote kuwazika, mabwana, mabibi, watoto; mabinti wote wataangamia kwa kuwa Nitamwaga hukumu kali kwa dhambi zao.”

Kwa hivyo waambie haya siku na mchana. Macho YANGU yatafurika na machozi. Siwezi kuacha kulia KWANGU kwa Watu WANGU wamedungwa na upanga na wamelala wakiwa na majeraha mabaya sakafuni. Nikienda kwenye viwanja, pale kuna miili ambayo upanga umeua. Na Nikienda kwenye mitaa, pale kuna miili imekufa na njaa na magonjwa. Na bado manabii na makuhani wote wameifanya kazi yao kusafiri kote nchini wakiwaambia watu kuwa kila kitu kiko sawa wakizungumza vitu ambavyo hawavijui.)

Hivi Ndivyo Asemavyo YAHUVEH, haya ndio Maneno YANGU ambayo hayawezi kunirudia MIMI tupu. Yatafanikisha ukweli kuwa MIMi sio Mungu tu wa huruma na upendo lakini Mungu wa ghadhabu kuu na kulipiza kisasi. Kulipiza kisasi ni YANGU Ndivyo Asemavyo YAHUVEH, kwa kuwa MIMI ni Mwenyezi katika utakatifu na Nilitoa njia ya kuepuka kupitia Mwana WANGU YAHUSHUA, lakini YEYE hudharauliwa na kukejeliwa na Jina LAKE linatusiwa na kulaaniwa au YEYE Anakataliwa. Ni Damu YAKE pekee inayoweza kuosha dhambi.

Ni wachache sana waliokubali Damu hii na hata wale wanaoikubali, ni wangapi huikanyaga na kuitupa kwenye sakafu, wakikejeli na kusema sasa Ninaweza kufanya kile ninachotaka. Ninaweza kuishi na mguu mmoja ndani ya Mbinguni kwa kusema ombi na mguu mwingine ndani ya jehanamu kwa kujihusisha na dhambi za dunia hii. Ninasema haya kwenu nyinyi wahudumu mnaofikiria kuwa mnaweza kuishi maisha yasiyo takatifu nyuma ya milango na nyuma ya akaunti za benki zilizofungwa. Wale ambao Ninawapandisha cheo pia MIMI huwashukisha cheo na Nitawainua wengine na kuwapa Baraka ambazo Nimezihifadhi kwa majina yenu. Kwa kuwa mna mfano wa utakatifu na hamna utakatifu ndani yenu. Wakati unakuja kuisha. Kwa kuwa maisha yenu hayataokolewa na watu watapata kujua siri mlizozificha, mifupa kwenye vyumba vyenu vya faragha ambayo mnayafufua kila siku.

Nyinyi mnaojiita wahudumu, lakini nyinyi sio wahudumu WANGU. Kwa kuwa sijali ni mafunzo yapi unayoamini au ni shule gani ya Bibilia ulipata digrii au ni nani anayekuheshimu. Kama hausimami kwa sababu ya utakatifu hamnihudumii MIMI. Hamjaitwa na YAHUSHUA MASIHI. Mmeitwa na mnayo mafunzo ya shetani na hamzungumzi juu ya vitu ambavyo vinakera, kwa hivyo hamzungumzi dhidi ya maisha ya dhambi, wala ushoga, au ponografia, au kuavya mimba? (Hamzumngumzii) utakatifu wa ndoa na onyo za usherati.

Hamzungumzi juu ya kuishi katika utakatifu. Haya tu ni ‘dini ya kujisikia vizuri’ na hamjanifurahisha MIMI hata kidogo. Jehanamu itakuwa zawadi yenu ya pekee na makofi mnayopigiwa hapa duniani. Mtateseka kwenye moto wa mateso wa jehanamu kwa kuwa uongo wenu haukuwapoteza nyinyi wenyewe lakini pia mliwapoteza wengine hadi jehanamu pamoja nanyi.

Yeremia 15:1-3 Kisha BWANA akaniambia: ‘‘Hata kama Mose na Samweli wangesimama mbele ZANGU, moyo wangu usingewaendea watu hawa. Waondoe mbele za macho yangu! Waache waende! Nao kama wakikuuliza, ‘Tuende wapi?’ Waambie, ‘Hili ndilo BWANA asemalo: “ ‘Wale waliowekwa kwa ajili ya kufa, wakafe, waliowekwa kwa ajili ya upanga, kwa upanga, waliowekwa kwa ajili ya njaa, kwa njaa, waliowekwa kwa ajili ya kutekwa, watekwe.’)“ Kwa wale wa magonjwa watakufa katika magonjwa yao na wote watajua wakati vitu hivi vitakavyokuja kufanyika nabii WANGU wa kweli amezungumza, kama vitu hivi havitafanyika, basi mtajua kuwa alitabiri kwa uongo. Na tena Ninawaambia vitu hivi anavyovizungumza vitakuja kufanyika na mtaishi kuona hofu hii ikija kufanyika. Lakini wale ambao ni WANGU, wasionikataa MIMI, wanaosimamia utakatifu, hata kama sio wengi wanakubaliana nayo, au ni gharama ipi utakayolazimika kulipa, Ninasema kwenu nyinyi, “Amini nabii na mtafanikiwa,’ na sasa tena Ninazungumza kwenu nyinyi, “Amini handmaiden huyu WANGU na kuwa ni RUACH ha KODESH Anayempa maneno haya kusikia Ninayoyazungumza na kwa sababu mmeyaamini haya, mtaepuka hofu ijayo.

Ninawapenda wale ambao wanaitwa kwa Jina LANGU, wakifanya amri ZANGU, wakiishi kwa utakatifu kama MIMI Nilivyo mtakatifu, wakioshwa kwenye Damu inayookoa ya Mwana WANGU Mpendwa, wakisaidia kusambaza unabii kwa wote mbali na karibu, wakihamasisha wale wanaozungumza vitu hivi kwa fedha na pia maombi yenu. Kwa kuwa hawawezi kufanya kazi kama dunia hii inavyofanya kazi, kwa kuwa lazima watoe wakati kuwa NAMI kusikia sauti YANGU, kazi yao ni kufanya yale huyu handmaiden na wengine wanafanya, dunia itafikiria kuwa hawafai kufanya kazi ya dunia, wala hawatakuwa na wakati wa kuifanya, kwa hivyo Ninawainua wengine ambao wataweza kufanya kazi na kutoa zaka na sadaka ili kuhakikisha kuwa Manabii WANGU wamelishwa na wana makao na wana fedha kusafiri na kuzungumza jumbe hizi wao wenyewe na katika upako WANGU, kwa kuwa muda ni mfupi.

Mnaona Niliwaambia, mna dakika moja hadi usiku kupitia huyu nabii lakini kile ambacho hamuelewi, ni nini kitafanyika kwa sekunde ya 59, 58, hesabu… moto wa mateso utakua moto zaidi. Mnahitajiana. Tena Ninasema msiwe pekee yenu. Lakini wengi wenu mnafikiria kuwa hamhitaji binadamu mwingine kuwalinda mnapoingia katika eneo shetani amenyakua kama zake. Kutaneni pamoja sanasana katika nyakati hizi za mwisho.

Kwa kuwa Ninawaambia haya, hamjui ni usiku mgani Ninapokuja, je, itakuwa saa sita usiku (12:00 am) au itakuwa sasa saba usiku (1:00 am) na kuna masaa mengi kabla asubuhi ifike, kwa hivyo ni saa gani Nitakapokuja? Tazameni na ombeni na MIMI Ninataka kuwaona mkifanya kazi ya Baba yenu wa Mbinguni, mkiishi kwa utakatifu kama Mungu wenu Alivyo mtakatifu au Nije na Niwapate mmelala kwenye kazi. Au nije na nyinyi ambao hamtaki MIMI kuja hivi karibuni, mko na mipango yenu na ajenda. Msijali, siji kwa sababu yenu!

Nimetoa onyo hii kwa kuwa tena Ninasema masaa ya usiku inawadia. Nisije MIMI kama mwizi usiku na Nikupate hauko tayari. Wale waouvu wataendelea kuwa waovu zaidi, na wale watakatifu watazidi kuwa watakatifu. Ninawatenga wale ambao wamewekwa kuenda mbinguni na wale waliowekwa kuenda jehanamu. Kutoka sasa kuna upanga wa kugawa na mtaniona MIMI Nikitenga uhusiano ambayo hapo mbeleni Niliruhusu. Lakini sio tena! Kwa hivyo msifikirie haya sio sawa mkiyaona yakija kufanyika.

Kwa sababu Ninawapenda, Nimewaonya, Nimewapa moyo na ndio siku hii upako ulio juu ya wale ambao wanaamini na kupokea haya kama Baba Mwenyezi Anavyozungumza kupitia huyu handmaiden watauhisi upako wa RUACH ha KODESH WANGU ukikorogwa ndani yao na mtatabiri kwa nguvu na kwa sauti ya juu na ujasiri zaidi kushinda hapo awali. Kwa wale wanaosoma haya na kusema, “Kweli mwanamke huyu ni mjinga, hakuna chochote kati ya haya kitakachofanyika.” Mtakuwa wa kwanza kuhisi joto na thibitisho la ghadhabu YANGU na kulipiza kisasi!

Imezungumzwa kupitia upako wa RUACH ha KODESH kwa chombo hiki cha udongo, Sherrie Elijah [Elisheva Sherrie Eliyahu] sio kwa nia nyingine ila tu kwa kuthibitisha kuwa MIMI huwatuma Manabii WANGU na maneno ya toba na kuepukana na maovu kabla ghadhabu za Mwenyezi YAHUVEH hazijakuangamiza.

Imezungumzwa, imeandikwa siku hii ya 5-25-98 ikamalizwa saa kumi na moja na dakika arobaini na tisa jioni (5:49 PM). Imezungumzwa, imeandikwa katika jina la YAHUSHUA MASIHI. Mtume Sherrie Elijah (Elisheva Sherrie Eliyahu).



CLICK HERE or the image below to go directly to her youtube channel
YAHSladyinred