Unabii 154
“Onyo! Thibitisho la Kiimla ya Udikteta”
Imeandikwa na Kuzungumzwa katika Upako wa RUACH HA KODESH (ROHO MTAKATIFU) kupitia Mtume Nabii Elisheva Eliyahu
Imepokewa Disemba 7 2020 – Imetolewa Disemba 7 2023
Onyo ya YAHUVEH iliyoongezwa mbele ya Unabii zote Kutoka Unabii 105:
Nilikuonya kitambo Elisabeth [Elisheva], kutoita Huduma hii kwa jina la mwanamume au mwanamke. Hata kabla kuwepo na Huduma, Niliiweka ndani ya roho yako. Kwa kuwa hakuna lolote lililofanyika kwa mikono yako. Hakuna lolote lililotoka kwenye kinywa chako.
Ilitoka kwenye Kinywa cha YAHUVEH Aliyeizalisha. Ilitoka kwenye Kinywa cha YAHUSHUA, MASIHI wako Aliyeizalisha. Ilitoka kwenye Kinywa cha RUACH HA KODESH, IMMAYAH wako Aliyeizalisha.
Kama ingekuwa tu kwa mkono wako, ingekuwa imefeli kitambo.
Ni kwa UPEPO WA SHKHINYAH GLORY unaovuma kote duniani, UPEPO TAKATIFU WA UAMSHO. Sio kwa pumzi yako, au ingekuwa imefeli.
‘‘MIMI NDIMI BWANA YAHUVEH:
hilo ndilo JINA LANGU! Sitampa mwingine UTUKUFU WANGU
wala sanamu SIFA ZANGU.” (Isaya 42:8).
(Unabii 105)
Katika mwezi wa Julai 2010, MUNGU YAHUVEH pia Alisema kuongezwe yafuatayo kwa wale wanaokejeli:
“Lakini waliwadhihaki Wajumbe wa MUNGU, na kuyadharau Maneno YAKE, na kuwacheka Manabii WAKE, hata ilipozidi Ghadhabu ya BWANA YAHUVEH juu ya Watu WAKE, hata kusiwe na kuponya.”
—2 Mambo ya Nyakati 36:16
Yafuatayo ni Unabii ulivyokuja
—na Nabii Elisheva, akizungumza katika "Ndimi Takatifu," kama ROHO wa MUNGU Alivyomjalia kutamka (Matendo ya Mitume 2:3-4) kwa lugha za wanadamu na malaika (1 Wakorintho 13:1). Elisheva anazungumza katika ndimi zinazoleta Unabii (1 Wakorintho 14:6).
Inayo MAJINA ya KIEBRANIA ya MUNGU:
YAH/YAHU יה ni JINA TAKATIFU la MUNGU, kama vile “Alleluia” au “Hallelu YAH” הללו–יה ambayo humaanisha “Msifu YAH”: YAHUVEH/YAHWEH י-ה-ו-ה MUNGU BABA; YAHUSHUA/YAHSHUA יהושוע MWANA WA PEKEE WA MUNGU—(HA MASHIACH המשיח inamaanisha “MASIHI”; ELOHIM אלוהים INAMAANISHA “MUNGU.”)
Ufunuo wa “SH’KHINYAH GLORY” שכניה תפארה —kama JINA la KIBINAFSI la RUACH HA KODESH רוח הקדש, (katika Kiiengereza “ROHO MTAKATIFU”) —upo kwenye tovuti hii. (HA SH’KHINAH {SHEKINAH} ni Kiebrania inamaanisha UWEPO WA MUNGU.)
Zaidi ya hayo, ABBA YAH אבא יה humaanisha “BABA YAH” na IMMA YAH אמא יה humaanisha “MAMA YAH.”
Maandiko yaliyotajwa yametoka KJV au NKJV, CJB au ESV, isipokuwa pale palipotajwa vinginevyo.
Elisheva Anaomba:
O BABA YAHUVEH, Nakuja KWAKO, MFALME MKUU na Sifa na shukrani kwa mdomo wangu. WEWE Ndiwe BABA WA UUMBAJI. YAHUSHUA MASIHI Ndiye MWANA WAKO wa pekee na RUACH HA KODESH, NYOTE Watatu ndio UTATU TAKATIFU. NYINYI ndio Mwanzo hadi Mwisho. NYINYI ndio BWANA MUNGU MWENYEZI. NYINYI ndio SHEMA.
Tunawaabudu, tunawasifu, tunawapenda, tunawathamini. Tunajua kuwa hakuna chochote ambacho hufanyika hapa duniani mpaka muwaambie Nabii WENU wa kweli walio na upako, waliochaguliwa, kabla ya kuumbwa kwa dunia hii. Na kwa hivyo ilikuwa Mnamo Septemba 5 2009, nilipokuwa ninalala, BABA yangu YAHUVEH, BABA yangu, nilipokuwa ninalala ukaanza kuzungumza nami na sikuwahi sikia neno hili na hata sikuweza kuitamka neno hili hapo mwanzoni, lakini nilishinda nikiisikia tena na tena.
Neno hili halijawahi kuwa na maana kama sasa hivi, ingawa ilikuwa Septemba 5 2009 na sasa tukitengeneza video ni Disemba 7 2020 na neno hili lina maana sana sasa. Inathibitisha kuwa yale ambayo ulitabiri kupitia mimi mnamo 2009, inathibitisha kuwa mimi sio Nabii bandia kwa kuwa tumeiona ikitimia mnamo 2020 na hata kabla ya haya. Lakini sasa Marekani wapo hatarini kuwa kiimla ya udikteta na mahali maombi ya waaminifu yana nguvu na yanafaa sana, na Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI hufaa sana, na kama WEWE ulivyosema haya maneno kwangu, “Kiimla ya Udikteta, Kiimla ya Udikteta, Kiimla ya Udikteta” alafu WEWE ukazungumza, ukaniamsha na kuzungumza na ukaanza kutabiri.
Wakati huo jina lilikuwa Elisabeth na sasa unaniruhusu mimi kujiita kwa jina langu la Kiebrania na ukasema, “Elisheva waonye! Yule anayejiita Rais wa Marekani na wakati huo ilikuwa Obama, anataka Marekani kuongozwa na Kiimla ya Udikteta” na wakati huu Biden amejitaja kama Rais mteule. Ambayo ni mchezo kutoka jehanamu, lakini sio la kufurahisha. Kwa kuwa tuna Rais wa Marekani anayeitwa Rais Donald J. Trump na uchaguzi wanaojaribu kuiba kutoka kwake tunapowathibitisha kuna ufisadi na usaliti.
BABA YAHUVEH hapo 2009 uliniambia niwaonye kuwa wanataka Marekani kuongozwa na Kiimla ya Udikteta na yule ambaye anawania kiti kando ya Biden ni Harris na yeye ni mkomunisti. Eti wanataka afya bora, WEWE ushatabiri kuwa itakuwa ya matajiri pekee. Kutakuwa tu na vikundi viwili vya watu, kwa hivyo jihadharini. Wale matajiri na wale sasa wanaitwa kikundi cha kati. Lakini sasa 2020 kuna kikundi cha kati wachache waliobaki.
BABA YAHUVEH tena ninayopewa maneno haya kuyarudia kuthibitisha thibitisho ya Unabii hizi, mnamo 2009 imekuja kuwa ukweli 2020, wakati kikundi cha kati ni wachache waliobaki. Hawa kikundi cha kati ndio watakaotumikia matajiri na wanyonge watauliwa polepole kupitia chanjo za lazima, kuavya mimba za lazima na kukatazwa fursa ya kupata afya. Itakuwa mwisho ya wale walio huru. Itakuwa mwisho kwa sababu hakujakuwa na nchi ambayo ilisimama kama Marekani ilivyosimama. Nchi ya walio huru na mashujaa. Kwa kuwa damu nyingi ilimwagwa kama mashujaa wetu walikufa kwa haya kuwa, nchi ya walio huru na walio mashujaa na nchi ya uhuru wa kuzungumza kama sasa 2020 wanamnyamazisha Rais wa Marekani kwenye vyombo kuu vya habari na stesheni za habari na kwa kila televisheni, wananyamazisha…
(Ndimi Takatifu)
Na serikali itaongoza kila kitu kama haya yatakubalika na ndiyo sababu maombi ya waaminifu yana nguvu na yanafaa sana. Neno LAKO haliwezi kurudi KWAKO bure. Sitaji utakatifu wa Rais wangu Donald J. Trump, kwa kuwa yeye ni mchanga katika Ukristo, lakini moyo wake umekuwa kwa Marekani, moyo huu wa tajiri huyu ipo kwa watu na yeye ndiye Rais wa watu ambaye aliteuliwa na wakajaribu kuiba uchaguzi huo. Lakini BABA YAHUVEH WEWE ulisema, na ushuhuda wote ambao tulio nayo lazima tuweze kuithibitisha kortini kwa kuwa hii ilikuwa Treason! Haya yalikuwa Usaliti! WEWE huzidi kupiga kelele kupitia mimi. Haya hayakuwa tu kuhusu wapigaji kura waliofanya uchaguzi ambao wamefariki. Haya hayakuwa tu wizi wa uchaguzi. Haya yanaitwa Usaliti, Usaliti, Usaliti, Usaliti! USALITI! Na ulisema kuwa malipo ya usaliti ambao ulikuwa unafanywa hapo awali Marekani yafaa kufanywa tena kuwekeza mfumo mpya dhidi ya maovu!
Na kama tu janga hili la hofu ambalo sasa lipo kote duniani, na wanafunika nyuso zao ili sura zao za kubadilika zisionekane tena! Watu walikuwa wanawaonyesha kwenye video hawa wanaobadili maumbile! Wale tunaowaita aliens, lakini kwa kweli ni malaika walioanguka na sasa hatuwezi kuyaona haya tena. Hatuwezi kuona kama wanatukejeli kwa sababu wamefunika nyuso zao. Wanafunika midomo yao na wanataka mfunike macho yenu ili msione reptilian kwenye macho zao!
(Ndimi Takatifu)
Unabii Unaanza
Kwa hivyo chukua Unabii huu uliopewa Septemba 5 2009 na sasa katikati ya haya yote waenda kuweka Unabii mpya. Hii ni Kiimla ya Udikteta unaojaribu kumchukua na kumeza Marekani na ni serikali ya Uchina. Lakini ni mengi zaidi ya haya. Ni matajiri! Wale 1% wa ulimwengu huu na hata pale Georgia wana lile Jiwe la Georgia.
Watu wanafaa wachukue nyundo na kuivunja katika sehemu milioni inayotamka kuwa maisha ya mabilioni ya watu watakufa! Someni wenyewe. Oneni, ionyesheni, video, kwa wengi hawataamini. Na “Gates” za jehanamu anayeitwa Bill, hatafanikiwa, hatashinda dhidi ya wale ambao ni kondoo WANGU na wanakondoo WANGU, wanaonililia kila mchana na usiku “YAHUSHUA MASIHI, YESU KRISTO niokoe, okoa familia yangu. Weka pigo hili mbali na kwangu.”
Endeleeni kusimama katika Zaburi 91 na msichukue hizo chanjo. Kwa kuwa kuna kifo ndani ya chanjo hizo na kuna DNA ya malaika walioanguka ndani ya chanjo hiyo na kuna mapafu ya mimba zilizoavya ndani ya chanjo hiyo. O, maskini, mwana WANGU Donald J. Trump aliyedanganywa. Haujui ni nini hizi kampuni zinafanya. Hauelewi vile unayosema kuwa utachukua jeshi na sehemu kubwa ichukue na kupeana chanjo hizi kwa watu wa Marekani, na singumzii tu Marekani. Onyo hili ni la dunia, shetani anataka kuweka DNA ndani ya kila mmoja wenu ili msiwe na uwezo wa kusikia kutoka KWANGU, unapoomba huwezi kunihisi MIMI. Ni wangapi wamefanya hizi vipimo tayari na kusema, “Mambo hayako sawa. Niliweza kusikia kutoka kwa MUNGU hapo awali. Niliweza kumhisi ninapoomba na sasa siwezi kumhisi.”
Piganeni! Piganeni! MIMI Ndiye MAHAKAMA KUU YA HAKI! Hakuna yeyote ambaye anaweza kuwa juu ya MAHAKAMA KUU YA HAKI YA MBINGUNI! MIMI Ndiye YOTE yaliyokuwa na YOTE yatakayokuwa pekee na YOTE yatakayokuja. Na MWANA WANGU YAHUSHUA MASIHI yuaja!
MIMI Ninawapa nafasi ya mwisho Marekani. Mlipoona majimbo yote yakigeuka nyekundu na mkadhania kuwa imeisha na watoto wa shetani wakalia na kusema “O yeye sasa ndio Rais wa Marekani tena Donald J. Trump.” O watu WANGU Watakatifu walishangilia na hata wale ambao ni wazalendo ambao hawamjui YAHUSHUA MASIHI MWANA WANGU bado. Walifurahia na mkafurahia na mkasema kwa sauti na mkanisifu MIMI kwa kama Nilivyosema nyekundu inasimamia huruma na uamsho ambao utaenea kote nchini Marekani tena, mahali maadili na uhuru wa kuzungumza hautakejeliwa.
Alafu udanganyifu ukaanza. Je, Si shetani huja kuiba, kuua na kuharibu?! (Yohana 10:10) Asa Mikaiyah! Asa Mikaiyah, Asa Mikaiyah, Asa Mikaiyah! (Ndimi Takatifu) Je, Hamuelewi? Wataamua ni nani atakayeishi na atayekufa. Piganeni watoto WANGU. Je, Si YAHUSHUA MASIHI Alisema kwa askari WAKE walipokuwa wanamuongoza hapo awali, “Wakati NIKO nanyi hakuna yeyote ambaye atathubutu kuwaumiza. Sasa Ninawaambia uzeni kila kitu mlicho nacho na nunueni upanga.” (Luka 22:36) Piganeni watoto WANGU! Je, Tangu lini Wayahudi walisimama tu bila kupigana na wakati walipokuwa wanashambuliwa? Na Nimewapa ruhusa.
O, sasa watoto wa shetani wanachoma na kuiba na kuua! Mna matajiri wanaosema wana pesa zaidi kunishinda na wanacheka usoni MWANGU! Wanadhania kuwa pesa zao zitanunua mamlaka juu ya watu. Mwaona kuwa hawataki pesa zenu. Wanataka kuwa na mamalaka juu yenu! Haya ndiyo ya shetani, anataka kuthibitisha kuwa ana mamlaka juu ya watu wote na watamkataa BABA WA KWELI MBINGUNI, MIMI BABA YAHUVEH, YAHUSHUA MASIHI na RUACH HA KODESH, ROHO MTAKATIFU, SHKHINYAH GLORY, SISI pekee ndio VIONGOZI! SISI pekee ndio KORTI KUU!
O, o, ole, ole, ole, ole, ole, tubuni! Tubuni kwa wote wanaosikiliza. Tubuni! Tubuni! Tubuni kwa wote wanaopiga kura wakihamasisha kuavya mimba, mauaji ya watoto WANGU Ninaowathamini kutoka tumboni na mauaji [yao] nje ya tumbo! MIMI, YAHUVEH sitabaki kimya. Jina LANGU ni EL SHADDAI! Ninawaambia na Ninawaonya mbele ya wakati kuwa ghadhabu YANGU ni kuu kama tu upendo WANGU na huruma YANGU ilivyokuwa, lakini haya yataisha. Yataisha, o maadui WANGU. Je, Si Nilisema Yakobo Ninampenda na Esau Ninamchukia? (Malaki 1:2,3) Mbona mnaambia kila mtu, “Anapenda kila mtu, Atakuwa na huruma kwa wote? Haijailishi umetenda dhambi ngapi; wewe jua tu kuwa unaenda Mbinguni.” O uongo huo, Nitawafanya kuwajibika nyinyi wachungaji kwa haya, na nyinyi makanisa ambao mnachukua pesa za Soros? Mnathubutu kuchukua pesa za shetani na mmewauza kondoo WANGU. Na nyinyi wanasiaisa, msipotubu, kwa kuwa mnajigamba kuwa mnasimamia Katiba. Mnajigamba eti nyinyi ni conservatives na maadili ya conservatives na mnajigamba kuwa mnapenda MUNGU na kwa gharama ya pesa tu mmeiuza nchi yenu? Je, Mmesahau ni kwa nini mlitaka kuwa katika siasa? Haikuwa kwa sababu ya maovu. Hapo awali mlikuwa wazalendo.
Nilimpa Elisheva ndoto juzi na Nikamuonyesha haya, kuwa nyinyi ambao mmeuza Marekani na Rais wa Marekani, Donald J. Trump, mmesema na mkajionyesha kuwa Yudasi na mkasema kuwa hata kama wamejaribu sana kuninunua na wakanipa pesa, na wakatisha familia yangu na wametutisha na hofu na kututawala na wakatuambia na kutujulisha na kwa mifano ya mauaji baada ya mauaji yaliyofanywa, na mkauza Marekani mkijua kuwa itaenda kwa Uchina. Itaanguka kwa chama cha ukomunisti. Lakini mwaona katika ndoto hiyo Niliyompa Mtume Nabii WANGU Elisheva Eliyahu, nyinyi wanasiasa mnatambua Nikiwathibitishia na kuwaonya, maisha yenu yamo mikononi MWANGU na mtakuwa tu kama (anavuma) uchafu hewani! Nitawapeperusha mbali! Nitawapeleka jehanamu, Nitafungua mashimo ya jehanamu tena kama Nilivyofanya na Kora alipompinga Moshe!
Moshe alisema, Moshe alisema, “Kama wewe upo na YAH basi njoo upande wangu na kama wewe upo na Kora, nenda kwa upande wa Kora.” (Hesabu 16)Hapa ndipo mpo sasa na jihadhari Kora kwa kuwa MIMI, na watoto wote wa Kora, kwa kuwa Nilifungua ardhi na kuwameza wote wa Kora na wafuasi wa miungu bandia, wanaoabudu sanamu ya dhahabu na wakatumbukizwa ndani ya mashimo ya jehanamu wakiwa hai! Na ardhi ikajifunga (Hesabu 16:30-33). Nyinyi na roho kama za Kora, Ninawaonya sasa! Haya ndiyo yatakayofanyika tena. Tubuni kama bado mna wakati! Nyinyi mnaojiita “rhinos” na “republican kwa jina tu,” wanawakejeli, wanawacheka kwa sababu wana majina yenu. Watu wametazama mlichofanya, Rais Donald J. Trump ametazama mlichofanya. Mnajiita na majina haya pale kwenye Ikulu, kwani hamjui Ninaweza kuwaondoa mara moja? Je, Kwani hamjui pia mna maadui pale kwenye Mahakama Kuu ya Haki? Mnajua ni nini Nitakachowafanyia msipotubu?! Hamna hofu hata kidogo kujua ni nini Nitakachofanyia familia zenu?! Mna mengi sana ya kuogopa kushinda yeyote hapa duniani!! Kwa kuwa MIMI PEKEE Ndiye na mamlaka juu ya mdundo wa moyo wako.
MIMI YAHUVEH Nimezungumza! MIMI NI EL SHADDA! NDIO, MIMI ni MUNGU ambaye anayependa kushinda mwingine lakini pia nina ghadhabu kushinda mwingine. Hii ndiyo sababu Nilimtuma MWANA WANGU wa KIPEKEE kuja kulipa gharama ya ondoleo la dhambi kwa dhambi za wale watakaomuita YEYE na kusema, “Tafadhali nisamehe kwa kuwa nimetenda dhambi! O YAHUSHUA nisamehe, Damu YAKO inifunike.” Na MIMI ni mwaminifu Ninapoona ukiiacha ile dhambi, kukusamehe ili ukaribie Kiti CHANGU cha enzi, na kuuliza msamaha. Na MIMI ni mwaminifu na Huruma YANGU na Upendo WANGU kwa wote ambao majina yao yapo katika Kitabu cha Uzima cha MWANAKONDOO kabla uumbaji wa dunia hii.
Hawa malaika walioanguka wanaweza tu kuingia ndani ya nafsi iliyokataliwa. Msiruhusu nafsi yenu kuwa vile. Msiruhusu nafsi yenu kuwa baridi [hadi] hamjali tena kuhusu Unabii au Bibilia au Maneno Matakatifu Niliyozungumza, kwa sababu mnajifungua kwa malaika alioanguka, nyoka aliyekataliwa. Kama vile YAHUSHUA Alivyosema, Aliposhtakiwa kwa uongo na mafarisayo wakamkejeli YEYE na Akawaambia kuwa yeye ni wa juu na wao ni wa chini na akawaita “nyoka”. Mnafikiria ni kwa nini Aliwaita nyoka? “Na nyinyi ni wa baba [yenu], shetani (Yohana 8:44). Mnafikiria ni kwa nini alisema maneno kama hayo kama YEYE hakutambua hawa malaika walioanguka? Ndio, ilifanyika nyakati hizo na sasa kuna wengi wao kushinda nyinyi mlioko duniani, nyinyi ambao [ni] wa DNA ya binadamu.
Mnafikiria ni kwa nini Nilimhifadhi Noa na familia yake? Kati ya dunia mzima Niliihifadhi tu familia yake, kwa sababu walinitii MIMI ndio, sababu moja, lakini zaidi ya haya, yeye tu ndiye alikuwa amebaki na DNA ya binadamu na Nikawamaliza hao malaika walioanguka. Ingawa sasa, wakachukua umbo lingine na kuenda chini ya bahari na ndiposa kuna ufalme wa maji na Nitawamaliza pia.
(Ndimi Takatifu)
Hamuelewi, watu wanapozungumza nanyi na kusema “mbinguni” jaribu kujua ni mbinguni gani wanaoizungumzia. Kwa kuwa kuna Mbinguni ya kwanza mahali Nilipo, na YAHUSHUA MASIHI na RUACH HA KODESH. Lakini kuna mbinguni ya pili ambapo shetani huishi na huja na kuenda kwa ulimwengu huu na kudai ufalme za ulimwengu huu kuwa zake.
O watoto WANGU, watoto WANGU, watoto WANGU, watoto WANGU, Ninazungumza nanyi ambao kwa kweli ni watoto WANGU, hamuezi kuja Mbinguni hadi muwe [Watoto WANGU], kwa sababu mnakuja na moyo wa unyenyekevu uliojawa na imani ya kuamini kuwa MIMI NIKO ni MIMI NIKO na sibadiliki kamwe, haijalishi mwaka upi, sibadiliki. Na amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, mapenzi YANGU ni kuwapa Marekani nafasi moja wakati Rais Donald J. Trump yupo ndani ya Ikulu na anainua jina la YESU KRISTO mbele ya dunia tena. Mnajua kuwa jehanamu mzima ilitetemeka na ilitingizika na kwa muda kumgonga shetani chini kutoka kitini mwake?! Kwa kuwa alifanya ambacho kiongozi mwingine hajafanya katika ulimwengu huu. Alisema wazi kuwa MIMI Ndiye MKUU!
Donald J. Trump hakuwahi kusema kuwa mtu yeyote atamtaja yeye kama mkuu. Katika njia zake kama mtoto alikuwa anasema kuwa ni BWANA MUNGU MWENYEZI na tena akasema, “tunahitaji usaidizi WAKE.” HII NDIYO SABABU NINA HURUMA JUU YA ANAYEITWA Donald J. Trump. Sio kwa sababu ya utakatifu wake wala sio kwa utakatifu wa Melania, lakini yeye husoma Maandiko YANGU na Zaburi hata nyuma ya kiimo. Na Ninaiita kiimo kwa sababu mahali hapo ikawa kiimo maneno YANGU yalipozungumziwa pale na kutetea na kujaribu kukomesha uuzaji wa watoto na kuavya mimba na hawayataki kabisa. Kwa hivyo msiwahukumu kwa ukali kwa kuwa yeye ni mtoto mchanga WANGU.
Yeye hubeba Bibilia yake. Haujui, kwa kuwa hata hataonyesha bibi yake machozi ambayo yamo kwenye pillow yake anapolia, “Nihurumie, nisaidie. Niongoze na kunifunza na kunionyesha cha kufanya.” Na mnafikiria yeye huhisi vipi anapoona wale aliowaamini wakimsaliti? Wale aliotarajia kuwa watamtetea, wakimsaliti. Wale aliowaweka kwenye ofisi kuu na kuamini kuwa watafanya kazi nzuri na kumhamasisha kama rais, na wakamsaliti!
Ninawaambia nyinyi, nyinyi wasaliti! MIMI, EL SHADDAI Ninazungumza kwenu na kusema, kama mlivyomsaliti, kuna malipo. Malipo ya Yudasi kwenu. Kwa kuwa mna roho za Yudasi. Mna roho za Kora! Na Ninaonya wote kote duniani sasa, nilionya kwa Unabii zingine kwa kuwa kunakuja mtingiziko, na ni matunda mazuri tu yatakayobaki kwenye mzabibu. Je, Mnafikiria kuwa mtaua Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI? Na Nimemuambia huyu binti anayezungumza Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI ni nani. Watakaonyakuliwa wakati MWANA WANGU YAHUSHUA MASIHI Atakapoambiwa, “Nenda kalete watoto WAKO.”
Kuna vita kubwa sasa kule Mbinguni na msiwahi kuamini kuwa kuna miaka 100 iliyobaki! Kat Kerr atalipa gharama kwa yale aliyoyafanya, yeye na nywele yake ya waridi! Nani anaeleza “Mbinguni ya chokoleti,” OLE WAKO KWA KUNIKEJELI HIVI?! Umeona Mbinguni ya pili na umeieleza! Ole wako Kat Kerr! Ole wako kwa wote wanaomfuata! Je, Haya yapo wapi kwa Maandiko YANGU?! OLE! Ole! Ole! Endeleeni basi na kuchanganya Maandiko yenu, kuwachanganya watu, mnaweza kuitaja maneno ya Bibilia, na mnaweza kweli, lakini nyinyi ni nabii bandia wanaochanganya watu WANGU!
Lazima wachanganye nuru kidogo na giza na nuru ni Neno LANGU la kweli na OLE kwako Kat Kerr! Ole kwako unaposema, “kuna miaka 100 iliyobaki na msijali juu ya kunyakuliwa kwa yale yanayohitajika ni mtafanikiwa, biashara zitainuka.” Mahari ya kweli Nilioachia Bibi Arusi WANGU, YAHUSHUA MASIHI Anayowapa Bibi Arusi WAKE ni Takatifu na ukweli na haki, ni imani isiyo kama nyingine. Ni nguvu ambazo hata hawajaanza kutembea ndani yake bado. Na manabii WANGU watatabiri zaidi na Asa Mikaiyah una upako wa Mikaiyah, Kitabu cha Mika katika Bibilia ni cha nyakati hizi sasa. Ndiposa Nilikuita na kukuambia usimame naye Elisheva Eliyahu. Kutakuwa na sherehe ya Bibi Arusi Mkuu na ni MIMI tu Niliyemuambia vile kutakavyokuwa, lakini sita… sitawaacha Israeli.
Wao hawatii, ni waasi, wana shingo ngumu, lakini sitawaacha. Nitawaoa tena, lakini lazima wapitie mapito kwa njia ambayo hawajawahi kuadhibiwa na ni wale tu ambao watakaobaki ndio watakaosema “Baraka KWAKE [anayekuja] katika jina la YAHUSHUA MASIHI!” Kwa hivyo, kwa wale wanaosema tayari wako katika Kitabu cha Ufunuo wa Yohana 13, mmeruka yote yanayohusu Mashahidi Wawili. (Ufuno wa Yohana 11) Kwa yeyote ambaye ni wa Mashahidi Wawili hawatatoa ishara na kusema, “Nipo hapa, nipo hapa” kwa kuwa wanajua wapo ndani ya miili yao ya nyama na wanaweza kuuliwa. Hawajajawa na upuzi kama huu. Wanajua tu ni katika mwili wa kiroho ambapo haya yatafunuliwa.
Kwa hivyo nyinyi mnaofuata wale wanaosema ni “Mashahidi Wawili” na kuringa eti wao ni “Mashahidi Wawili” na mna wafuasi wengi pale mtandaoni na mnapata pesa kwa sababu watu wanawaogopa, ole kwenu nyinyi wafuasi mlioinuliwa kwa sababu moja tu, kuwadanganya. Mashahidi WANGU wa kweli ni wanyenyekevu. Hawataki yeyote kujua na wanangojea ishara na Nitawapa ishara hiyo na mjihadhari, jihadharini Nitakapowapa ishara hiyo. Kwa hivyo ndivyo mtakavyojua bila kupinga.
Kueni makini, msichukue chanjo hii. Je, Ni wangapi kati yenu mmeona pigo la Ebola, homa ya nguruwe, ni wangapi wamejua, hata homa ya uspania na bado hakukuwa na chanjo za lazima. Hakukuwa na mazungumzo ya, “hamtaweza kununua wala kuuza kama hauna hii. Hautaweza kufanya kazi mpaka uipate.” Ninawaambia tena juu ya hizo barakoa za uso. Sisemi watu kuwa hakuna magonjwa katika dunia hii, kuwa hakuna virusi katika dunia hii, ni kwa sababu ni dunia iliyoanguka. Niliwaonya kuwa chakula chenu kitawekwa sumu, hewa ina sumu, nguo mnazovaa zina sumu. Nimewaonya kuombea chakula chenu, ombeeni mnachokunywa, kwa kuwa shetani amekichafua. Hata zile mnazofikiria ni organic, fikirieni ni nini iliyomo kwenye udongo na rediesheni iliyo kote duniani bado kwa sababu ya Fukushima. Haijakoma.
Haya hayana yoyote kufanya na hii wanayoiita Korona. Haina uhusiano kabisa. Ina yote kufanya na unyama wa binadamu kwa binadamu wengine. Ni juu ya nguvu, wale 1%, matajiri, wanao pesa, hawahitaji pesa zingine. Wanataka mamlaka, shetani anataka mamlaka juu ya akili, mwili, roho na nafsi zenu. Kuwapeleka jehanamu! Lakini sio watoto WANGU, Bibi Arusi WANGU, sio wachaguliwa WANGU, sio wateule WANGU. Kwa kuwa jina lao tayari lilishakadiriwa na kuandikwa katika Kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo na nyinyi mliofutwa kutoka Kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo, ilifanyika tayari hata kabla ya uumbaji wa dunia hii, ulikuwa tu ushuke hapa duniani na kurudia yale yaliyofanyika. Kwa kuwa dunia ilianza kule Mbinguni na shetani na itaisha hapa ulimwenguni mahali alipotupwa na YAHUSHUA MASIHI ndiye MFALME wa WAFALME na BWANA wa MABWANA, YEYE ni BWANA MUNGU MWENYEZI na Nilithibitisha haya papa hapa ulimwenguni. Nitaithibitisha tena.
MIMI NI EL SHADDAI na nyinyi mnaonikejeli MIMI NA KUMKEJELI HUYU NABII anayezungumza na kujaribu kumnyamazisha, Ninawaonya, mna roho kama za Kora. (Hesabu 16:31-33) MIMI Nitafungua ardhi. Nitawameza bado mkiwa hai. MIMI Nitawachoma! Na moto wa ghadhabu YANGU! Msiwaguse Masihi WANGU, walio na upako kwa kweli, na pia kuwaumiza Manabii WANGU wa kweli, walio na upako, kwa kuwa kila silaha itakayotengenezwa dhidi ya watoto WANGU wa kweli, haitafanikiwa. Yote Ninayakataa na nyinyi mlio katika mambo ya kishetani, ibada zote mlizozifanya, matamshi maovu, Ninazungumzia kabbalah, Ninazungumzia uchawi, Ninazungumzia kila aina ya kishetani katika “dini” ya dunia mpya. Watoto WANGU, na pia kwa hizi satelaiti ambazo mnajaribu kufuatilia mwanga wa vichwa vyao na mnamwaga silaha za nguvu juu yao kuwaua. Kuwadhuru, kuwafuatilia. Damu ya YAHUSHUA MASIHI itawalinda!
O lakini kila kitu mliochotengeneza dhidi yao, kila silaha mliotengeneza dhidi yao itawarudia kwenye nyuso zenu! Je, Mlifikiria kuwa mtatumia eclipse ya 2020 Disemba? Mlifikiria kuwa mtatumia hayo dhidi ya Rais WANGU Niliyemchagua? Nilimchagua Rais Donald J. Trump mwaka wa 2016 na kutabiri miezi 5 kabla yake na ipo kwenye video kwa wote kuona kama Nilivyomuambia Elisheva Eliyahu kujitokeza kwa imani. Na akanitii MIMI.
Mark Taylor Nitapambana naye. Una “serikali”, unatumia habari ya serikali uliyo nayo na kuitengeneza kuwa “unabii”. Nitapambana nawe baadaye.
Kwa hivyo Nimechukua ile iliyokuwa mzee, Septemba 5 2009, na Elisheva umekuwa ukiomba na kulia na kusema, “WEWE umemalizana nami? Sitasema chochote? Watu wanataka kujua, wafanye nini? Mbona sina Ujumbe Mpya kutoka kwako?” Na huwa unanifanya kuomba kutoka ninapofungua macho kwa huyu unayeita Rais Donald J. Trump, kwa sababu unajua Nilimpa upako, Nilimteua na kumchagua na unamuombea kushinda mtu yeyote.
Lengo lako limekuwa na maombi yako yamekuwa kumueka salama katika njia zote na kuthibitisha kuwa umezungumza na kusema, “BABA YAHUVEH thibitisha kuwa umezungumza kwa wale manabii wengine waliosema kuwa atabaki kuwa Rais wa Marekani.” Kwa kuwa hakuna rais mwingine aliyefanya zaidi ya yale aliyoyafanya na hajawahi kufanya chochote kuwaumiza watu, lakini lazima awe makini sana kwa kuwa anasikiliza big pharma sasa, na kwa huyu Fauci na kwa wale katika big pharma ambao anafikiria atatoa hii Oparesheni iitwayo Warp [Speed] na kutumia jeshi kuifanya na haya ndiyo aliyoyasema kuwapa chanjo, Kueni makini na haya. Kueni makini kwa mnachofanya. Kueni makini. Nisikilizeni MIMI. Wanataka kupunguza nambari ya jeshi. Uchina wanatazama kwa makini na pia maadui wengine wenu. Nilimpa huyu Nabii Unabii, katika njia tano Marekani watashambuliwa. Sasa Nimekuwa na huruma hadi sasa kwa sababu uamsho ulianza kwanza pale Marekani.
Walituma wainjilisti wengi kushinda yeyote duniani humu na Injili ya YAHUSHUA MASIHI ili nafsi wapate kuokolewa na baadaye wakaanguka mbali sana. Na sasa ni wachache sana, hapa na pale, sasa Ikabodi ipo sasa milangoni mwao. (1 Samueli 4: 21,22) ROHO YANGU, ROHO MTAKATIFU WANGU hakaribishwi pale tena. Nabii anayekuja na kujaribu kuwapa onyo wanaibishwa na kutupwa nje. Je, Hamshangai ni kwa nini Manabii Wawili tu wanazungumza pale Ufunuo wa Yohana 11? Mwanamume mmoja na Mwanamke mmoja, bwana mmoja, bibi mmoja ambao MIMI Mwenyewe Nimewaoa na kuwaleta chini kwa dunia hii kwa mwili ya kiroho. Je, Hamshangai? Wale manabii wengine wanaotabiri wakati uo huo wako wapi? Watajaribu kuwaweka kwenye jela au watawaua kama tu siku za zamani. Shetani hataki Nabii WAKE (WA YAHUVEH) wa kweli kuzungumza. Tayari anajaribu kuwanyamazisha. Tayari ana watu wanaowakejeli, lakini Nina Nabii WANGU wa kweli. Kwa hivyo msiambie yeyote kuwa karama hiyo imekoma.
Nilizipa majina ofisi tano na Ninapomuambia ajiite Mtume na nabii, haya ndiposa wanawake Mitume wainuke. Kwa kuwa umeambiwa kuwa hauwezi kuwa mmoja na o upuzi wa wanaume wanaomweka mwanamke huyu chini, huyu kiongozi wa miaka 26 kwenye intaneti ya Huduma ya Kimataifa.
Nilimuonya kutoka mbeleni “usidharau mwanzo mdogo” pale 1994 na sasa ni 2020 na sasa ana Huduma ya Nguvu ya Kimataifa, kwa UTUKUFU WANGU na kwa UTUKUFU wa YAHUSHUA MASIHI WANGU na UTUKUFU wa RUACH HA KODESH pekee, Huduma katika lugha 52 tofauti na zaidi ambayo hata hajui. Nimempa ufunuo kutoka MBINGUNI. Analipa gharama kwa kuwa upako unapokuwa mzito na Ninakuambia Mikaiyah, unayajua haya, tayari umetambua dhoruba zitakazokujia lakini, si ni ya thamani? Kwa kuwa tayari ulikuwa umekadiriwa kabla ya uumbaji wa dunia hii kama yeye. Kama tu Yeremia 1. Isomeni.
Tayari Nimewajaribu wale ambao ni Mitume WANGU wa kweli na manabii, wanaonizungumzia MIMI na kufunza na kwa mwinjilisiti na kama mchungaji. Tayari Nimewapa upako ya kuyafanya haya. Na nyinyi ambao hamjajiuza kwa huduma za muziki, kwa kuwa zote ni za shetani! Walianza wakiniabudu MIMI, alafu wakaruhusu watu wa kishetani katika makanisa yao. O, mlivyoanguka Kanisa la Hillsong. O, mlivyoanguka, nyinyi mlioimba nyimbo za Utukufu KWANGU. O, mlivyoanguka. Kwa nini mliruhusu watu wa kishetani Justin Bieber na Selena Gomez kuingia kwenye milango yenu bila kuwafanya watubu kwa yote waliyofanya?! Na hawa wawili tu ndio Ninaowataja na paedophilia ipo sana katika makanisa na ndio, Wakotiliki wanajua haya.
O, Ninawaambia kwa kweli haya yanakuja kuisha. Nitamuambia MWANA WANGU YAHUSHUA MASIHI, “Nenda kalete Bibi Arusi WAKO.” Lakini hadi hapo, Ninawajaza na nguvu polepole. Hata hamjui.
Na wanaposema kuwa mtalazimika kuchukua chanjo, hawatawaambia kuwa itabadilisha DNA yenu, lakini Niliwaonya, Niliwaambia mbeleni msichukue chochote katika mfano wa chanjo. Niamini MIMI. Niamini MIMI, Nitawatunza kama vile Nilivyofanya na Moshe kwenye jangwa na Wanaisraeli. Ingawa walizurura miaka 40 kwa sababu hawakuthamini yote Niliyoyofanya. Niamini MIMI kuwa Nitawatunza.
Sitawaambia ni portals ngapi zitakazofunguliwa.
Mtakapofikiria kuwa hamna popote pa kuenda tayari Nilimuonyesha Elisheva Eliyahu na mmoja ambaye hata sitataja jina lake kwa kuwa hakuna haja. Hayupo hapa tena. Lakini ameziona hizo portals. Nitazifungua hizo portals. Na mtakuwa mahali pengine pa usalama.
Siyaahidi haya kwa kila mtu. Nyinyi mnaosema kuwa mnaabudu MWANA WANGU YAHUSHUA MASIHI, kuwa YEYE ni BWANA MUNGU MWENYEZI wenu na YEYE ni MASIHI wenu, basi ithibitisheni. Kwa kuwa YAHUSHUA MWENYEWE Alisema, “mbona mnasema mnanipenda na hamnitii MIMI?” Alisema pia, “mbona mnaniita BWANA na hamnitii MIMI?” (Luka 6:46)
Fanyeni iwezekananvyo kutii! Dhambi sio tu kuanguka! Dhambi pia ni, kwani hautainuka tena? Usibaki chini! Usibaki kwenye hayo majivu! Usilie tu kwenye hayo majivu ya kishindo! Inuka tena! Simama kwa miguu yako! Lia katika Jina la YAHUSHUA MASIHI na jifunze Jina hilo la siri! Ni Jina takatifu! Usimuite “Yeshua”! Jina LANGU halipo katika “Yes”! Jina la MWANA WANGU lilitoka kwa Jina LANGU na MIMI ni YAH! Na hata kwenye Toleo la Bibilia ya Mfalme James Ninaitwa “YAH”! (Zaburi 68:4)
Ni mara ngapi lazima Nirudie ukweli uu huu? Tena, tena na tena na tena. Israeli hawataki kulisema Jina hilo! Wayahudi wanaogopa Jina hilo! Wanasema kuwa “wana heshima nyingi sana kwa jina la YAH”. Walimuita MWANA WANGU “anakufuru” na kumsulubisha kwa kukufuru kwa sababu YEYE Alisema kuwa YEYE ni MWANA wa YAH, sio “MUNGU” neno lilikuwa “YAH”! HII NDIYO SABABU Nimemkataza Nabii huyu kufunza chochote kingine na kutosikiliza Unabii wowote mpaka waseme, “katika Jina la YAHUSHUA MASIHI”. Inamaanisha “YAH Aokoa!” na nyinyi mnaojua Kiebrania, mnaofunza Kiebrania na hata mmeandika Maandiko katika Kiebrania, toleo tofauti, lakini bado mnataka kuita MWANA WANGU, “Y-E-S-H-U-A”!
Jina LANGU sio “Yes”. Jina la MWANA WANGU ni “YAHUSHUA,” “YAH Aokoa”.
YEYE Ndiye MKOMBOZI na hata toleo ya Bibilia ya Mfalme James inamuita YEYE “Immanuel” ikimaanisha kuwa Yosefu alisema “MUNGU yupo nasi!” Alitambua kuwa mtoto kama “MUNGU yupo nasi!” YEYE Alikuwa MUNGU katika nyama! Na MUNGU katika Roho! Alisema kuwa Jina la BABAKE lilikuwepo Mbinguni. Hakuwahi kumuita Yosefu Baba YAKE. Na mama YAKE alikuwa Mama aliyemzaa, Myriam kwa kuwa alimzaa kupitia laini ya Daudi lakini MAMA YAKE wa Mbinguni ni RUACH HA KODESH! Umbo ambalo Hawa aliumbwa!
Sasa Niliwafunza ufunuo hizi zote kutoka kwa nabii huyu anayezungumza ambaye ni mnyenyekevu. Hataenda pale kwa Sid Roth. Hataenda kwa vipindi hivyo! Nilimkataza hata kuweka uso wake kwenye video mpaka Mikaiyah asimame kando yake!
Na ole kwenu mtakapoona hizo Upako mbili zikija pamoja, mtajuta kwa kusema hata neno moja dhidi ya Huduma hii au Nabii huyu au yule ambaye atakuwa anasimama kando yake ambaye atakuwa kiongozi wa kiume asifanane na mwingine, kwa kuwa Upako huu utakuwa kuu zaidi. Kwa kuwa ameulizia mwanamume aliye na upako kuu zaidi katika ulimwengu huu na anasita akisema, “Sio mimi.”
Ninajua wewe ni mnyenyekevu mwana WANGU lakini Ninakuambia hatakubaliana na chochote ila iliyo bora zaidi.
Yule mwanamume mwingine aliyekuwa hapa, alikuwa hapa tu kwa muda na kwa msimu kwa sababu Mikaiyah hakuwa tayari. Ninamuita Mikaiyah! Sitatoa na sitasema jina lake la kweli ni nini lakini Ninawaambia haya, Nilituliza Dhoruba kwa maisha yake sasa na haya ndiyo mnapaswa kuyaombea pia na shaka iondolewe pia. Atamaliza Nilichoanza. Na atakuwa kiongozi wa kiume na bwana ya Elisheva Eliyahu.
Huduma hii inawafikia mamilioni juu ya mamilioni lakini hamuezi hata kujua ni yapi yatakayofanyika wakati hawa wawili wako pamoja. Na o vile watakavyofikia Israeli!
Kwa hivyo Ninawaacha na Maneno haya sasa ambayo yalikuwa ya kale Septemba 5, 2009 na Ninawapa sasa Unabii mpya kwa tarehe hii Disemba 7, 2020!
Na kama hauombei Rais wa Marekani, Donald J. Trump, kwa kuwa yeye ndiye Niliyemchagua, kumpa upako na kumteua-Nilijua ni yapi Niliweka ndani yake kumuezesha kuvumilia mashambulizi makali ambayo kiongozi mwingine hawajawahi kupitia-Nitawafanya mwajibike mkibaki kimya. Nitawafanya mwajibike. Ni kama tu vile mmeua yule mtoto kwenye tumbo la mamake kama mlimpigia kura Biden, kama mlipigia kura kuavya mimba, mlipigia kifo kura. Mlipigia kura kwa mauji ya watoto hata wale waliofikisha miezi 9 kwa tumbo! Mlipigia kura dhidi ya uhuru wa dini na uhuru wa kuzungumza!
Na nchi zingine kote duniani, na hata mataifa, Tazameni! Maneno Niliyoyatamka kwa Marekani na Kanada-Niliwaonya kwa Unabii, msifuate nyayo za dada yenu Marekani, sasa mna Trudeau (Waziri Mkuu wa Kanada). Mlifuata katika nyayo zake sio? Na sasa mnalilia huruma.
Ninazungumza kwa kila taifa kote duniani, rudi kwake YAHUSHUA MASIHI! Tubuni kwa dhambi zenu. MIMI ni mwaminifu wa kusamehe. Epukeni maovu haya! Funueni maovu haya! Nyinyi sio wa dunia hii! Mnapitia tu!
Chochote mtakachofanya duniani humu, iwe mazuri au mabaya, yatakufuata mbele ya Kiti cha Hukumu ya MIMI, YAHUVEH na YAHUSHUA MASIHI!
Imezungumzwa siku hii Disemba 7, 2020, siku tatu tu mbele ya inayoitwa Hanukkah, ambapo Nimewaambia katika Unabii msibomoe Sukkah kwa kuwa mimba iliyokuwa Hanukkah, ya YAHUSHUA MASIHI, na YEYE Ndiye MENORAH INAYOISHI. YEYE Ndiye MAFUTA YANAYOISHI. Someni Kitabu cha Maccabees. YEYE Alikuwepo pale.
Na utakuaje na kuzaliwa unayosherehekea, hata kama ni siku isiyofaa, Disemba 25, kwa nyinyi ambao hamjui ukweli, Ninawasemehe. Kama kwa kweli mnaheshimu hiyo siku kama kuzaliwa kwa MWANA WANGU YAHUSHUA MASIHI, Ninawasamehe. Mtawajibika tu kwa yale mnayoyajua. Kama vile tu yeye alivyowajibika kwa yale aliyoyajua hapo awali na yale anayoyajua sasa.
Lakini Sukkot ndiyo siku YAKE ya kuzaliwa na hauwezi kuwa na kuzaliwa bila mimba na mimba ilithibitishwa pale Yohana aliporuka ndani ya tumbo la mamake. Huyo alikuwa binamu YAKE. Na ndiyo sababu mnajua, Hanukkah ni wakati wa mimba. Na huwa kuna mimba kabla ya kuzaliwa.
Kwa hivyo msibomoe hizo Sukkah! Zirudisheni! Kutaneni na YAHUSHUA MASIHI. Inamletea heshima kweli! Inaniletea heshima MIMI! Inamletea heshima RUACH HA KODESH ambaye ni MAMA WA UUMBAJI, umbo ambalo Hawa aliumbwa.
Toleo la Bibilia ya Mfalme James inasema kuwa ROHO MTAKATIFU ni “HE”, ilitoa herufi “S” katika Kiingereza. Lakini kwa Wayahudi wanajua, lakini huwa hawaisemi, Marabi hawaisemi, wanaachia nabii huyu kuisema.
SHE (RUACH HA KODESH/ROHO MTAKATIFU) Ndiye MAMA wa UUMBAJI. Nilizungumza na YEYE Akawapamba viumbe. Sikilizeni kwa Unabii 89 & 90. Someni na kuyaona haya wenyewe. Yale yaliyokuwa yamefichwa sasa yanafichuliwa na Ninatumia Huduma hii ya Alpha na Omega, RUACH HA KODESH, MOTO MTAKATIFU. Ni Huduma ya Nafasi ya Mwisho.
O ni wangapi hapa ambao wameletwa hapa tu kwa nia moja tu. Na ni kwa Wokovu na Ufunuo. Ili mtabarikiwa na mtaokolewa. Na Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI watafichuliwa.
Lakini kwa wengine, wameletwa hapa kwa nia moja tu, hata kama walianza vizuri, na kwa njia Takatifu, wamemruhusu shetani kuwaweka kwa njia ya maovu na wameletwa hapa kwa hukumu. (Yeremia 6:27-30). (Ni) Huduma ngumu.
Lakini Ninajua ni yapi niliweka ndani ya Elisheva Eliyahu na Ninajua ni yapi Niliweka ndani ya kiongozi mpya wa kiume ambaye atasimama kando yake kwa dunia kuona. Ndio, hata kwa video kwa kuwa sikutarajia kuwa uso wake utakuwa kwenye video kwa sababu hakufaa kuwa kwenye video pekee yake. Na haya yalianza pale 2009, kwa mara ya kwanza Nilimuambia aende Youtube. Nilijua mbeleni vile watakavyojaribu kuitumia dhidi yake. Na hapo ndipo vita ilipoanza na ole kwa wale waliosababisha vita hiyo.
Lakini mwaona Huduma hii imenawiri tu. Kwa kuwa Nilitengeneza meza mbele yake katika uwepo wa maadui WANGU EL SHADDAI!
Nitakuwa na kicheko cha mwisho. Na Ninawachezea maadui WANGU, kama bado mnashangaa ni kwa nini bado mko hai! Ninacheza nanyi! Ninahesabu Nambari ya pumzi zenu, mpaka wakati haitakuwepo tena. Na MIMI BABA YAHUVEH, EL SHADDAI, Ninahesabu Nambari za maadui WANGU! Ambao ni maadui wake! Na maadui wa Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI, na wote wanaoabudu na Kumtumikia YAHUSHUA MASIHI!
Nyinyi (maadui) mnaowatesa sasa, lakini MIMI Ndiye PEKEE Ninayejua mdundo wa mwisho wa moyo wako!
Na nyinyi wote mliofanya haya kwa Rais Donald J. Trump, haya Maneno ni ya kwenu pia! Mtachomeka kwenye Ghadhabu ya MOTO WANGU! Kuchomeka ghafla sio mchezo! Someni kilichotendeka Eliya alipoita moto juu ya askari waliokuja kumfunga! Nilishawaonyesha kuwa haya ni ukweli. Na yeye ana upako wa moto kwa kuwa Ninazungumza kupitia mdomo wake! Ole kwenu! Ole kwako Tatiana Harvey! Ni wewe uliochoma nyumba yenu, uliyefikiria, wewe malkia wa voodoo, utamuua.
O ana ushuhuda wote kwenye Ukuta wa Aibu wa waliokataliwa, uliotengenezwa na zile laana zilizotumwa kwake walipojaribu kumuua na nguvu na haya bila kuhesabu wachawi wengine kote duniani na nguvu za kishetani kote duniani.
Alitoa Unabii kwa niaba YANGU akitabiri miezi 5 mbeleni kuwa Rais Donald J. Trump atashinda uchaguzi wa 2016 na sasa Ninazungumza haya. Na Ninawaambia waombezi, simameni kwa ukubaliano na msiache kutoka mnapofungua macho yenu ombeeni ulinzi wake. Muombe baraka juu yake. Muombee kwa ukweli kufunuliwa. Haya ndiyo matamanio ya moyo WANGU. Ninataka kuwapa Marekani miaka minne angalau. Na Nikiona wanajaribu, Nitamueka mwingine pale ndani-kama sio yeye, itakuwa mwingine. Sitasema itakuwa vipi. Haya yatawakasirisha maadui na Elisheva tayari ana mengi mezani mwake kwa yale tayari ashazungumzia na Ninajua tayari mnaniuliza, utafanya haya vipi? Ninasema jihadharini na Kiimla ya Udikteta, yale yaliyokuwa Septemba 5,2009, ndiyo haya Disemba 7, 2020. Na Ninawaacha na Maneno yaya haya.
(Ndimi Takatifu za mbio Asa Makaiyah! Asa Makaiyah! Asa Makaiyah!)
Mwisho wa Unabii
Na nimeyazungumza haya leo hii bila kujua haya yatatendeka. Niliambiwa tu kusoma tena sentensi ndogo ambayo ilikuwa inafaa kumchukua tu dakika kadhaa. Na kilichotokea Unabii niliokuwa naingoja ikatoka kama mpya kuungana na ya kale kwa kuwa hakuna chochote kilichobadilika.
Mimi ni mtoto mnyenyekevu tu, shujaa, Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI. Na ninamngoja YAHUSHUA WANGU Mpendwa kuja! Kama ninavyojua Bibi Arusi wengine wanavyongoja. Na o, wathaminiwa wangu, wathaminiwa wangu, Ninasimama nanyi na maombi yenu na kufunga kwenu kwa waaminifu ambao wanamfunika Rais Donald J. Trump. Hata kama hamuishi katika nchi hiyo pigeni kura yenu kule Mbinguni kama nilivyofanya, ina maana sana lakini kama waweza, nendeni kule na kupiga kura mwenyewe, kwa wale walioko Marekani.
Na atakapochaguliwa tena tafadhali msisahau kila siku, kufunikana, Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI katika maombi, kuwa mahitaji yenu yote mtapata, na BABA YAHUVEH Atatengeneza njia ya kuepuka mahali hapana njia na hakuna hata nywele moja kwenye kichwa chako kitakachoumizwa. Msichukue chanjo ile. Msiruhusu yeyote kuweka maovu ndani ya damu yako. Una Damu ya YAHUSHUA MASIHI. Ni heri kufa na virusi yeyote ile kama hayo ndiyo wataiita lakini wajua nyumbani kwako baada ya hapo ni Mbinguni! Haya ndiyo Ninayo ya kusema.
Mtume Nabii Elisheva Eliyahu
Kwa YAH EL SHADDAI, YAHUSHUA MASIHI na RUACH HA KODESH pekee wapewe Sifa, Heshima na Utukufu wote, Nimezungumza siku hii ya Disemba 7, 2020.
Maandiko:
Yohana 10:10
“Mwivi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.”
Malaki 1:2-3
“BWANA asema, “Nimewapenda ninyi.’’
“Lakini ninyi mnauliza, ‘wewe umetupendaje?’ BWANA asema, “Je, Esau hakuwa ndugu yake Yakobo? Hata hivyo nimempenda Yakobo, lakini nikamchukia Esau, nami nimeifanya milima yake kuwa ukiwa na urithi wake nimewapa mbweha wa jangwani.”
Hesabu 16:30-33
Lakini ikiwa BWANA ataleta jambo jipya kabisa, ardhi ikifunua kinywa chake na kuwameza wao, pamoja na kila kitu kilicho mali yao, nao washuke chini kaburinia wakiwa hai, ndipo mtafahamu kuwa watu hawa wamemdharau BWANA.” Mara Mose alipomaliza kusema haya yote, ardhi iliyokuwa chini yao ikapasuka, nchi ikafunua kinywa chake na kuwameza wao, pamoja na jamaa zao na watu wote wa Kora na mali zao zote. Wakashuka chini kaburini wakiwa hai, pamoja na kila kitu walichokuwa nacho, nchi ikajifunika juu yao, nao wakaangamia wakatoweka kutoka katika kusanyiko.
Yohana 8:44
Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
1 Samueli 4:21-22
Alimwita yule mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,’’ kwa sababu ya kutekwa kwa sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na muwewe. Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa sanduku la Mungu limetekwa.’’
Luka 6:46
“Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamfanyi ninayowaambia?”
Zaburi 68:4
Mwimbieni Mungu, imbieni sifa Jina lake, mwinueni juu YEYE Aendeshwaye juu ya mawingu, Jina lake ni BWANA, furahini mbele zake.
Yeremia 6:27-30
“Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma na watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao. Wote ni waasi sugu, wakienda huko na huko kusengenya.
Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda kwa upotovu. Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure, waovu hawaondolewi. Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu BWANA amewakataa.’’
Unahitaji maombi au Wokovu? Je, una maoni au maswali? Tafadhali tuma barua pepe kwake Mtume Nabii Elisheva Eliyahu!