Unabii 75

MIMI, YAHUVEH, Nitawasafisha Na Kukutana Nanyi Ndani Ya Sukkot Yenu!

[Ninawaamuru Kufuata Na Kuheshimu Siku ZANGU Takatifu]

Imepewa kwake Mtume Elisabeth Elijah (Elisheva Eliyahu)

Agosti 27, 2004

Haya maneno yanatoka kwenye Unabii wa 105, YAHUVEH Alisema yaongezwe kwenye Unabii zote kutoka sasa: Nilikuonya kitambo Elisabeth [Elisheva], kutoita Huduma hii kwa jina la mwanamume au mwanamke. Hata kabla kuwepo na Huduma, Niliiweka ndani ya roho yako. Kwa kuwa hakuna lolote lililofanyika kwa mikono yako. Hakuna lolote lililotoka kwenye kinywa chako. Ilitoka kwenye Kinywa cha YAHUVEH Aliyeizalisha. Ilitoka kwenye Kinywa cha YAHUSHUA, MASHIACH wako Aliyeizalisha. Ilitoka kwenye Kinywa cha RUACH HA KODESH, IMMAYAH wako Aliyeizalisha. Kama ingekuwa tu kwa mkono wako, ingekuwa imefeli kitambo. Ni kwa UPEPO WA SHKHINYAH GLORY unaovuma kote duniani, UPEPO TAKATIFU WA UAMSHO. Sio kwa pumzi yako, au ingekuwa imefeli. (Isaya 42:8)

Katika mwezi wa Julai 2010, MUNGU YAHUVEH pia Alisema kuongezwe yafuatayo mbele ya Unabii zote kutoka Kitabu cha pili cha Mambo ya Nyakati:

2 Mambo ya Nyakati 36:16, “Lakini waliwadhihaki Wajumbe wa MUNGU, na kuyadharau Maneno YAKE, na kuwacheka Manabii WAKE, hata ilipozidi Ghadhabu ya BWANA juu ya Watu WAKE, hata kusiwe na kuponya.”

* * * * * * *

O Hazina ya moyo WANGU, hauamini kuwa MIMI, YAHUVEH, na Mwana WANGU YAHUSHUA tutawalinda mnapotazama Wakati huu Takatifu? Je, siwezi kuwalinda? Hata pale Yerusalemu, ambapo hatari ni kuu zaidi watu Waebrania wametengeneza Sukkot zao kama ilivyoandikwa kuwa wataniamini MIMI, YAHUVEH, kuwalinda na MIMI hufanya vivyo hivyo.

Je, mnaogopa kumkera nani MIMI, YAHUVEH, au majirani wenu? Je, mnajali ni yapi ambayo wengine hufikiria juu yenu kushinda ni nini kitakachonifurahisha MIMI, YAHUVEH, na YAHUSHUA? Hamjui ya kwamba Watu WANGU huitwa watu wa kipekee, kwa kuwa hawatembei kwa sauti ya dunia hii lakini kwa sauti ya Mbinguni? Mbona unaibishwa na haya, Mpendwa WANGU, kwa kuwa haya yatanishuhudia MIMI kwa Utukufu wa YAHUVEH? Ombeni majirani wenu waone haya ili mwaambie hadithi ya kwa nini nyinyi hujenga Sukkot kwa ukumbusho wa Neno LANGU. Haya yatanifurahisha, kwa kuwa wale wanaofanya haya hunishuhudia MIMI kwa majirani wao na Ninawauliza mfanye vivyo hivyo. Je, mtanishuhudia MIMI vipi na kuwa mfano wa imani yenu kama mtaficha Sukkot yenu ndani ya bafu?

Sukkot inafaa iwe nje mahali ambapo mnaweza kuona Anga. Wayahudi hata hawajatambua kwa nini Sukkot ina nafasi kwenye paa. Haya yanatekeleza maandiko haya “Angalieni Juu kwa kuwa ukombozi wenu wakaribia kwa kuwa YAHUSHUA MASIHI Atakuja kutoka upande wa kulia wa Anga” Msiogope maadui wanaowaumiza kwa kuwa MIMI, YAHUVEH, Nitawabariki na kuwalinda wale ambao ni WANGU na kuwaaibisha wale wanaodhani wana hekima, wanapoacha njia za dunia hii mbovu na kupuuza vicheko vya adui. Nitawakejeli wale wanaowakejeli katika wakati wao wa taabu.

Tengenezeni Makao ya muda mfupi inayo nafasi juu kuona Anga. Niulize MIMI na Nitawaongoza na kuwaonyesha vile vya kufanya. Kuleni ndani ya Sukkot yenu na kupumzika katika mikono ya MIMI, YAHUVEH, na YAHUSHUA. Nitakutana nanyi pale. Kwa wale wanaosema lazima wafanye kazi za dunia hii, Ninawaambia basi mpande mbegu zenu katika kazi ya Ufalme wa Mbinguni na mwone kama MIMI sitamwaga Baraka kuu ambayo itawapa sababu ya kusifu MIMI, YAHUVEH, na YAHUSHUA. Niliweka katika moyo wako, Binti YANGU Patricia, kuuliza maswali haya na kumwandikia Ringmaiden huyu wa YAHUSHUA ili atoe haya kwa wengine ambao ni wapya katika Sherehe za Kiyahudi na wana hamu ya kuyatimiza. Mnamtumikia MASIHI Aliyefufuka. Si mnafaa kufanya kama Alivyofanya Yeye kuheshimu na kuzifuata Siku Takatifu za Kiyahudi? Wale ambao wamechaguliwa kuwa Bibi Arusi wa YAHUSHUA husikia yale Nabii WANGU huandika MIMI, YAHUVEH, Ninavyompa maneno haya.

Yaliyo mazuri kwake YAHUSHUA sio mazuri kwa wale wanaomfuata YAHUSHUA MASIHI? Baraka zaja kwako Binti YANGU kwa kutii na kuandikia Elisabeth [Elisheva] na maswali haya, kwa kuwa sasa wengine watajifunza nawe pia. Neno hili linapaswa kutolewa kwa wote na macho ya Kiroho ya kuona na masikio ya Kiroho ya kusikia. Wote wengine watabaki viziwi na vipofu kama vile mafarao na mafarisayo wa nchi hii.

MIMI, YAHUVEH, Ninawapa Watoto, Bibi Arusi, Waliochaguliwa na Wateule WANGU, wanaokula Nyama ya Kiroho na kunitambua MIMI, YAHUVEH, Ninazungumza kupitia huyu Binti na kupitia kwake Ninatoa amri hii kwenu. Mnapaswa kusherehekea Siku Takatifu zote za Kiyahudi na siku zijazo za Sukkot kama kumbusho kuwa mnaishi katika Makao ya Muda Mfupi. Dunia hii ni makao yenu ya muda mfupi mpaka mje nyumbani Mbinguni. Wewe ni mpita njia tu mpaka utakapomaliza kazi uliyotumwa duniani kufanya. Maangamizi yaja hapa duniani, pamoja na kifo na maradhi na maafa ya hali ya hewa iliyosababishwa na binadamu anayejifanya kama Mungu. Mnapaswa kusherehekea Sukkot hata kama hujawahi kusherehekea hapo awali. Mnafaa kusherehekea Siku hizi zote Takatifu. Mahali imani yenu itakapokuwa, ndipo Pasaka yenu itakapokuwa. Mnafaa kufunga wakati wa Yom Kippur, mkinyenyekea mbele ya MIMI, YAHUVEH, na kufunga kwa sababu ya maovu yaliyomo nchini ili mweze kuepuka wakati kifo kitakapowatembelea maadui WANGU waliojiweka dhidi ya yote yaliyo Takatifu.

Mjikumbushe, mnapojenga Makao ya Muda yasiyokuwa na nguvu, vile Nyumba yoyote iliyotengenezwa na binadamu, haina nguvu. Upepo mdogo tu unaweza kuigonga lakini wakati MIMI, YAHUVEH, na Mwana WANGU YAHUSHUA tupo ndani ya nyumba hiyo isiyokuwa na nguvu, hata katika Hekalu hiyo isiyokuwa na nguvu iitwayo mwili wako, Nina uwezo wa kuwalinda wale Ninaowaita Watoto, Bibi Arusi, Waliochaguliwa na Wateule.

Nijaribu MIMI, YAHUVEH, na mtazame, Watoto, Bibi Arusi, Waliochaguliwa na Wateule WANGU, muone kama sitawabariki na kuwalinda na hata upako mkuu, wale wanaojitahidi kunipenda, kunitii na kunitafuta MIMI, YAHUVEH, na YAHUSHUA MASIHI.

Je, yaliyo mazuri kwake YAHUSHUA kuheshimu, sio mazuri kwako? MIMI, YAHUVEH, Ninawakumbusha. Hamwabudu na kumtumikia Masihi wa Kikristo lakini YAHUSHUA Alizaliwa kutoka kwa Bikira Mwebrania katika mchanga wa Kiebrania, Alitembea na kufunza ishara, maajabu na miujiza katika mchanga wa Kiebrania. YAHUSHUA Alifuata Torah na hakuwa na dhambi yoyote. YAHUSHUA Alifunza kama Rabi katika Sabato ya kweli ya pekee.

YAHUSHUA hakuhubiri katika Hekalu Jumapili. Wale na Masikio ya Kiroho ya kusikia, sikieni. Wote wengine wabaki viziwi. Kwa kuwa Sabato ni daima na milele itasimama kwa kuwa MIMI, YAHUVEH, Niliumba dunia hii kwa siku 6 alafu katika siku ya 7 MIMI, YAHUVEH, Nilipumzika na Nikaamuru mwanadamu kufanya vivyo hivyo. Mwana WANGU YAHUSHUA Aliitakasa Sabato na YEYE huitwa Bwana wa Sabato. YEYE ni mfano wa vile vya kuitakasa Sabato. Mwana WANGU Mpendwa YAHUSHUA Aliteswa na kusulubiwa na maneno yaliyokuwa juu ya kichwa chake, hakuna shetani yoyote au binadamu yeyote aliyeweza kuondoa na YAHUSHUA Akafa na kufufuka kwenye mchanga wa Kiebrania kutoka kwa kaburi ya Kiebrania.

Sasa Nilivyosema haya yote, kuthibitisha kuwa YAHUSHUA ni MASIHI Myahudi Aliyefufuka, msifuate njia za wapagani na msizifuate sherehe za makafiri ambazo YAHUSHUA hakufuata. Kama hayapo kwenye Maandiko Matakatifu, mbona mnanikasirisha MIMI, YAHUVEH, na kuyaongezea Maneno YANGU na kufunza kwamba siku za wapagani zinafaa kuheshimiwa lakini wanadharau kufuata siku MIMI, YAHUVEH, Nimekadiri kama Takatifu na za kukumbukwa kama wakati wa kale?

Mnanialika MIMI kwenye siku zenu za mwanadamu na kwa nini nyinyi husema kuwa nyinyi hunifuata, kunitumikia, kuniabudu, kunitii YAHUVEH na YAHUSHUA na mnatoa visingizio, kuwa vitu hivi ni vya Watu Waebrania pekee? Je, wewe sio Mwebrania kupitia kukubali Damu ya Mwana WANGU YAHUSHUA pale Kalvari, kama YEYE pekee Alivyokuwa Dhabihu ya Damu kwa dhambi zenu?

Je, hamwamini kuwa YEYE huishi sasa ndani yenu kupitia RUACH ha KODESH? Kumjua Mwana WANGU YAHUSHUA kwa undani, lazima upate kujua Uyahudi wa MASIHI Aliyefufuka. Mbona mnasisitiza kumwita YAHUSHUA ‘Yesu Kristo’ badala ya Jina LAKE la Kiebrania, YAHUSHUA, ambalo ni kumbusho ya kila mara kwake shetani kuwa YAH huokoa. Mbona mnasisitiza kugeuza maandiko katika Bibilia kutoa visingizio, kwa nini hamna Heshima kwa Siku ya Sabato ya Kweli na kuitakasa mbele ya MIMI, YAHUVEH?

Je, ni vigumu sana kuitenga siku ya Ijumaa Machweo hadi Jumamosi Machweo na kutambua kuwa hii ndiyo Siku ya Sabato na kuitakasa? Unapokosa kujua una kisingizio, lakini baada ya kujua ukweli na hamwachi ukweli kuwaweka huru na kusema kuwa hampo chini ya utumwa wa amri za kale, ni amri gani mnayotaka kutupa nje kwa sababu inawahangaisha? Kwa sababu tu wengine hawataweza kuelewa. Mnapoenda kanisa za Jumapili na hampo pale kumwambia Mchungaji na shirika kujua kuwa wanakosea kwa kutofunza Uyahudi wa MASIHI Aliyefufuka, basi MIMI, YAHUVEH, Ninawaita nyote waoga na mtawajibika.

Ninawatuma nyinyi kuwaonya wengine na mnapuuza yaliyo kweli. Mniabudu MIMI siku 7 za wiki na mkutane pamoja kama mnataka lakini mpe YAHUVEH Heshima kwa kutambua Siku ya Sabato na kuitakasa na kupumzika kutoka kwa kazi zenu katika siku hii na kuifurahia NAMI. Siku hii haifai kuwa kama mzigo lakini iwe ya furaha. Je, haya ni magumu kwenu? Ninawapa Siku Takatifu za Sherehe kusherehekea isipokuwa Yom Kippur, Siku ya Upatanisho ambapo mnafaa kufunga na kukumbuka gharama YAHUSHUA Alilipa kwa dhambi zenu. Je, haya ni magumu kwenu kweli kujifunza Siku hizi Takatifu za Kiebrania?

Ningechagua YAHUSHUA Azaliwe kutoka nchi yoyote lakini MIMI, YAHUVEH, Nikawainua Watu Waebrania kwa kubariki ukoo wao. Nyinyi mnaokubali damu ya YAHUSHUA sasa nyinyi sio mataifa na hamfai kufuata njia za wapagani au siku zao za sherehe. Lakini fuateni Siku Takatifu kama vile MIMI, YAHUVEH, Nilivyokadiri kuwa Baraka kwenu. Mmewajibika kwa yale myajuayo sasa, mtakachofanya nayo sio jukumu la Binti YANGU Elisabeth [Elisheva], jukumu lake ni kuwaletea maneno haya MIMI, YAHUVEH, huzungumza kupitia kwake. Haya sasa ameyafanya. Utakuwa msaada kwake au kizuizi? Kwa wale wasomao haya na maneno mengine MIMI, YAHUVEH, na YAHUSHUA tumezungumza na mmebarikiwa mlipojifunza kutoka Huduma hii ya Kitume na Kinabii ya nyakati za mwisho, lakini bado hamfanyi chochote kuwa Baraka kwake pia na Huduma hii, basi umekuwa kizuizi na MIMI, YAHUVEH, Nitawawajibisha kwa kufanya kazi yake iwe ngumu zaidi na mzigo kuwa mzito zaidi. Ni wangapi kati yenu humwuliza ainue majina yenu mbele ya MIMI, YAHUVEH, na kuniuliza MIMI, YAHUVEH, kuwabariki na kuwaombea. Anapofanya haya MIMI, YAHUVEH, huangalia majina ambayo yeye hutaja kwa maombi na MIMI, YAHUVEH, huwa makini. Je, walichukua wakati na kutoa dhabihu ambazo zitabariki Huduma hii?

Ninaibika Ninapoona wachache sana wakisaidia kwa njia yoyote. Wanachukua wakati kuulizia Baraka na bado hawaulizi ni nini wanachoweza kumfanyia yeye. Kwa kila wakati jueni haya, kila wakati alipoomba, “Tafadhali tutumie wasaidizi kutusaidia katika Huduma hii,” na mliweza kumsaidia kwa njia fulani na mlikataa, mkitoa visingizio, hii ndiyo nambari ya maombi Nitakayokataa mnaponiuliza MIMI, YAHUVEH. Kila wakati mliposikia mahitaji ya Huduma hii na mkafunga masikio yenu, na wengine Niliowatuma kwa Huduma hii wana utajiri wa dunia hii, na bado mnafunga masikio yenu kwa huyu Nabii WANGU, mnamfanya alie, basi Nitawafanya mlie MIMI, YAHUVEH, Ninapokataa malalamiko yenu iliyoletwa mbele YANGU.

Ni wangapi kati yenu mnaoweka majina ya watoto wenu au wapenzi wenu au familia kwenye agano la urithi (will) na bado hamjali Huduma hii inayowalisha? Ni wangapi wasomao haya sasa wana kazi, nyumba zaidi ya moja, ardhi, mali, vitu vya kale, mashua, ndege na pesa mnazoziweka kwa ajili ya ulafi kujiridhisha nyinyi wenyewe. Si Neno LANGU husema, “Mahali moyo wako ulipo, ndipo hazina yako itakapokuwa?” Mmenionyesha MIMI nyoyo zenu zipo wapi. Kila mtu aliyeongozwa hadi kwa Huduma hii anaweza kufanya kitu lakini wengi hawafanyi chochote. Je, mbona mwampa anayekuletea chakula cha mwili pesa (tip) na hampi chochote huyu anayeteseka kuwa na upako Niliyompa kuwalisha Chakula hiki cha Kiroho. Je, ni gani iliyo na thamani kuu? Chakula cha mwili kinachokusaidia tu kwa masaa kadhaa alafu una njaa tena au Chakula cha Kiroho ambacho utakikumbuka kila wakati na kukitafuna, sanasana katika nyakati ambazo mtahitaji kukombolewa au kutiwa moyo.

Ni kisingizio gani mtakachotoa mtakaposimama mbele ya MIMI, YAHUVEH, katika wakati mfupi tu ujao? Mmeonywa; wale wanaombariki huyu Binti Myahudi hawambariki tu yeye lakini MIMI, YAHUVEH, na Mwana WANGU YAHUSHUA. Elisabeth [Elisheva] ndiye Ninayemwita Eliyah WANGU Mpya [katika Kiebrania, Eliyahu]. MIMI, YAHUVEH, Nimemtuma kwa Wajane wa Zarepta na hawakujua. Nyinyi mnaokataa kusaidia kwa kiwanja hiki cha mavuno kote duniani hamna mahitaji ya kifedha sasa, lakini yaja. Nilimtuma Eliyah wa Zamani [katika Kiebrania, Eliyahu] kuwa Baraka kwa mjane mmoja, ingawa nchi hiyo ilikuwa na wajane wengi kutoka kwa ukame na njaa. Nilijua mbeleni kuwa mjane huyo atahitaji baraka na alikuwa tayari kumpa chakula chake cha mwisho nabii aitwaye Eliyah [katika Kiebrania, Eliyahu] hata kama alikuwa ameamini kuwa yeye na mwanawe watakula na kufa. Aliishi na alibarikiwa kifedha na chupa yake ya mafuta haikuisha. MIMI, YAHUVEH, Ninayo hamu ya kufanya yaya haya kwenu. Sio kwa bahati tu mmekuja kwa Huduma hii na mnayasoma maneno haya sasa.

Nitawabariki na kuwalinda nyote katika njia msizozifikiria, wakati maangamizi na majaribio yatakapokuja, kama mtatii yote MIMI, YAHUVEH, Ninasema Leo. Mzitakase Siku Takatifu za Kiyahudi mbele ya MIMI, YAHUVEH. Nikumbushe MIMI katika Pasaka mnaposherehekea na kuutoa chachu kutoka kwa nyumba zenu kama Nilivyowalinda Watoto wa Israeli walipoiweka damu ya mwanakondoo kwenye viimo vya milango yao, Nitawalinda zaidi wote walio na Damu ya YAHUSHUA ikiwafunika na nyumba zao. Katika Sukkot mnapotengeneza makao yenu ya muda mfupi, itakuwa ishara KWANGU vile mnavyonitegemea MIMI, YAHUVEH, kuilinda Miili yenu, kwa kuwa ndani yake huishi Roho zenu na RUACH ha KODESH WANGU, ROHO MTAKATIFU, kama mlivyo wageni katika Makao haya ya Muda Mfupi iitwayo dunia na mnapitia tu kufika Nyumbani kwenu iitwayo Mbinguni.

Mwishowe, wale wanaoishi Marekani, Nimempa huyu Nabii WANGU onyo kuwapa nyinyi. Nilimpa amri kutoa ndoto Niliyompa na yatafanywa. Ninajua wale na karama ya utambuzi wanamwangalia George W. Bush na wanajua ana mfano wa Utakatifu lakini hana Utakatifu ndani yake. MIMI, YAHUVEH, Nawaambia, George W. Bush ndiye afadhali kati ya waovu wawili. Mnajua ni nini kisicho kizuri na George W. Bush, lakini bado hajapuuza maneno fulani, ingawa kuna msukumo juu yake kupuuza msimamo wake, Makamu wa Rais Cheney akimsaliti tena. Cheney hana aibu na humtetea binti yake shoga aliyekataliwa kama jina lake linavyosema amefungwa kwa minyororo (chains) kwenye mfalme wa giza.

George W. Bush anasimama dhidi ya kuavya mimba, utafiti wa stem cell, chukizo chafu KWANGU kama vile ushoga na ndoa za jinsia moja. Msimdharau, Geoge W. Bush atashinda katika uchaguzi wa rais ufuatao, kwa kuwa Nilivyomwambia Binti YANGU katika ndoto, mnaposimama na kukosa kufanya chochote na msipopiga kura na kuomba, Democrats watashinda Uchaguzi wa Rais ufuatao na damu itamwagika katika nchi hii na wasiokuwa na hatia watawekwa gerezani, kwa kuwa watashtakiwa kwa hatia ambazo hawakuzifanya. John Kerry na bibi yake ni watumishi wa shetani, msidanganyike, na hawatajifanya kuwa watakatifu. Mmeonywa. Ninawaonya sasa John Kerry na bibi yake watawafanya mjute kwa nini hamkusikiliza Nilipowaonya kupitia huyu Binti WANGU wa Kinabii. Oneni picha hii, wale waovu na waliokataliwa wakishangilia katika Siku ya Uchaguzi. Wale mbwa mwitu katika ikulu wanajaribu kujificha lakini watavua barakoa zao siku hii, hakutakuwa na mwisho wa maovu yatakayofanywa na kwa kupotea kwa uhuru kwa wale wanaogopa YAHUVEH na YAHUSHUA.

Msisahau; haya yataathiri uhuru wa dini zote, hata Waislamu. Wote wanaotumikia miungu bandia lakini wana hamu ya kuwa na tabia nzuri watajuta hawakufanya chochote lakini walisimama na kutazama tu. Nyinyi ambao ni waombaji, anzeni kusisitiza kuwa Wachungaji wenu waache kupuuza ukweli na wazungumze hata wagharamike.

Kejeli kuu la Jina LANGU litafanywa na Ellen DeGeneres kwa kukufuru kuu kuniiga MIMI, YAHUVEH, Mungu wa Viumbe. Atalipa na nafsi yake kwa haya na wote watakaohusika katika filamu hii. MIMI, YAHUVEH, Nitatuma ghadhabu ZANGU kwa wale wajiitao wakubwa hadi kwa wale wadogo. Hawa ni Studio, Mzalishaji, Waandishi, Waigizaji, Wanaotengeneza nguo, Wanaoandaa chakula; Wajuzi wa make up, hata waigizaji wa kuongezwa. MIMI, YAHUVEH, Nitamwaga Ghadhabu ZANGU katika Jimbo hili mahali filamu hii itakapotengenezwa. MIMI, YAHUVEH, Ninaonya kila mtangazaji. MIMI, YAHUVEH, Nitawaamuru Watoto, Bibi Arusi, Waliochaguliwa na Wateule WANGU hata wale ambao hawanitumikii wala kutii Neno LANGU Takatifu lakini wanajua kuwa kuna Mungu YAHUVEH wa kuogopa, kuandamana na kukataa bidhaa zenu.

Mwanamke aitwaye Ellen Degeneres atanikejeli MIMI, akijifanya kuwa Mungu Mwenyezi. Yeye sio shoga tu kwa uwazi lakini yeye ndiye wa kwanza Marekani kupokewa na Ikulu akiwamo Rais wa U.S.A., walipotengeneza karamu yake na mpenzi wake wa jinsia moja ambaye alisema amemwoa. MIMI, YAHUVEH, Ninaita Ellen Degeneres, Ellen Degenerate (mwovu). Yeye amekataliwa na hana aibu anavyotuzwa na shetani na mali na umaarufu kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kudai ndoa ya jinsia moja na hana aibu na analipenda jina lake. Anzeni kuandamana na kususia na kuonya wote watakaosikia, yeyote atakayetazama filamu hii na kumsikia akikejeli MIMI, YAHUVEH, na hataandamana kwa kuogopa, atavuna alichokipanda.

Nilitabiri kupitia Binti YANGU Elisabeth [Elisheva], na unabii huo umewekwa kwenye mtandao kwa miaka sasa kwa wote kusoma [Unabii 20], Ellen DeGeneres aliwalisha watoto na watu pepo ya ushoga na akicheka. Kwa ajili ya haya MIMI, YAHUVEH, Nilitabiri kuwa yeye ndiye atakayekuwa wa kwanza kuonja Pigo la Damu Nyeusi na atalia akitaka kufa damu nyeusi itakapokuwa inamwagika kutoka mdomoni mwake. Wote washerati wataugua pigo hili la nyakati za mwisho. MIMI, YAHUVEH, Nilitabiri kupitia huyu binti YANGU kwa sababu Nilijua bwana yake Ellen DeGeneres, shetani, atakachomwelezea afanye na hii ni kukejeli Muumba wa Viumbe vyote.

* * * * * * *

Iliandikwa na kuzungumzwa siku hii ya 8/27/04. Ilipewa kwake Mtoto, Shujaa na Bibi Arusi wa YAHUSHUA MASIHI, Mtume Elisabeth Elijah (Elisheva Eliyahu).

Hii ndio Maadhimisho ya 16 ya Silaha ya Kiroho niliyopewa iitwayo GONGO la YAHUVEH. Mnaweza kusoma haya katika ukurasa wa ushuhuda wangu, sanasana katika “Upako Mkuu Maishani Mwangu pale Maui, Hawaii”. Nilipokuwa ninaandika unabii huu Baba YAHUVEH Alivyokuwa Akinipa, nilidungwa na nyuki. Shetani hajafurahia kuwekwa kwa neno hili kwenye mtandao na kwa kujaribu kunizuia mimi akitumia nyuki ni ujinga sana, yachekesha.

Soma barua pepe kutoka kwa Patricia iliyokoroga upako kwa neno hili kutoka.


* * * * * * *