UNABII 49

JIHADHARINI, NYINYI NI KAMA KONDOO WANAOONGOZWA KWENYE KICHINJIO!

Imeandikwa/Imezungumzwa katika upako wa RUACH ha KODESH kupitia Mtume Sherrie Elijah

Oktoba 1,2001

* * * * * * *

Ole kwa Kanisa na Hekalu ZANGU, ambazo hawafunzi watu kuomba dhidi ya vita Marekani, hii Vita vya Dunia vya 3 vitaangamiza kila taifa katika dunia hii. Kama hamfanyi haya msijiite kanisa. Usijiite Mchungaji WANGU, Nabii, Mtume, Mwalimu, kwa kuwa hausikii kutoka kwa upako WANGU kama hauwezi kuyasikia haya sasa hivi. Viongozi wa kiroho, mtanijibu ‘MIMI NIKO’, YAHUVEH kwa kukosa kuwaongoza watu waombe dhidi ya vitambulisho na uvamizi wa faragha. Mtawajibika kwa kukosa kuzungumzia dhidi ya uhuru na faragha yenu kuchukuliwa. Mnapeana bure. Je, Marekani hawajui ni gharama ipi walilipa kupata uhuru huu? Kwa kuwa hamtaiona ikirudishwa tena hadi YAHUSHUA arudi tena baada ya Dhiki Kuu.

Wachungaji, Ole kwenu. Sanasana wale ambao mna mengi ya kufaidika katika macho yenu, kwa kuwa mnachukua hali ya msamaha wa kodi yenu na mnajiuza kwa mkandarasi mkubwa. Nyinyi ni kahaba katika macho YANGU. Nyinyi kanisa ambazo hamzungumzi, wala kuwaambia Watu WANGU kuwa ilikuwa Vibaya, katika siku mlioita mkutano, siku ya makumbusho na maombi, mlimhuzunisha RUACH ha KODESH WANGU (Roho Mtakatifu) sana, hamfunzi, wala kuzungumza onyo. Ni dhambi kuomba kwa MUNGU mwingine ila YAHUVEH tu na YAHUSHUA (Yesu). Haya ni makosa na hamkujulisha serikali juu ya haya, vile maadui katika mataifa mengine wanavyowakejeli nyinyi Marekani. Kwa kuwa hakuna mahali pengine ila Marekani tu ambapo haya yangetendeka. Mlikuwa mmetengwa Marekani, kwa Utukufu WANGU, na sasa mnasema, “mungu yeyote aweza kujibu maombi.” Mmehatarisha nafsi. Mtajibu siku moja kwa haya mbele ya kiti CHANGU cha hukumu.

Aibu kwenu, wote mlionyamaza na kutofanya chochote kujaribu kuondoa aibu hii yaliyofanywa hewani. Ili MIMI Baba yenu MUNGU YAHUVEH Nisikasirike na Marekani tena, Niliiweka kwa akili ya Pat Robertson, kuwaombea wachungaji, lakini hakusema ni kwa nini Niliyafanya haya. Anajua kuwa wachungaji walikosea na bado aliogopa kuwakasirisha zaidi ya kunikasirisha ‘MIMI NIKO’. OLE KWA WACHUNGAJI Marekani na wote kote duniani, Ninawashauri, ‘Acheni kujifanya kama waoga.’ Usijiite Mchungaji, Nabii, Mtume, Mwalimu, Mwinjilisti, Kiongozi wa kiroho kama wewe ni mwoga. Jiuzulu sasa kabla hujawajibika zaidi kwa kuwapoteza kundi. Acheni kuwafunza Watu WANGU kupuuza ukweli kwa kuwa siku za kale walipigania haki ya kunitumikia ‘MIMI NIKO’. Wale waliofuata YAHUSHUA waliuawa lakini hawakupuuza ukweli.

Kanisa LANGU, inukeni tena na muwe Hekalu hai ya RUACH ha KODESH WANGU. Acheni kuwalisha Kondoo WANGU na wanakondoo pabulum, chakula kinachofaa watoto wadogo. Aibu kwenu. Nitawawajibisha, nyinyi wachungaji mnaopuuza ukweli na hamsemi maovu kama yalivyo. Wale watakaopuuza ukweli hawatarithi Ufalme wa Mbinguni. Mnawaogopa madikoni wenu, shirika, na serikali zaidi ya ‘MIMI NIKO’. Je, Nitawezaje endelea kumwaga Baraka ZANGU, na ulinzi kama mwaendelea kupuuza yale ambayo mwajua ni ukweli, imesimamishwa na Bibilia Takatifu na maandiko.

Ninawasihi nyinyi Wachungaji na kuwashtaki sasa. Aibu kwenu! Mmezungumza yale ambayo serikali, shirika, wale waliowanunua, wanawaambia mseme. Wachungaji mmepeana onyo kuwa mgaidi wa Marekani ni nani, lakini hamjapeana onyo kuwa adui wa YAHUVEH ni nani, na adui wa kweli wa Watoto WANGU, jina lake ni shetani na shetani huja kwa mifano nyingi sana, katika dini mbalimbali. Shetani anawaingiza katika vita ambavyo anajua itasababisha mataifa yote kuhusika katika njia moja au nyingine. Jihadharini, mtakapotaja tena Vita vya Ulimwengu vya 3, hivi ndivyo itakavyokuwa. Marekani, mnadanganywa. Amkeni Watu WANGU na mzungumze dhidi ya haya, mpe moyo Rais wenu kutafuta njia nyingine mbadala ya amani kuliko vita ambavyo vitahusu vita vya kibiolojia na viini. Hivi sivyo vita vya risasi. Hivi vitakuwa vita vya hali ya juu vitakavyotingisha Dunia hii na kwa kweli maneno Vita vya Ulimwengu vya 3 havitawahi kusahaulika, wala taifa lolote kubaki sawa. Mmeonywa.

Marekani, mnaniudhi MIMI na nyimbo zenu za MUNGU Bariki Marekani. Je, ni MUNGU mgani mnayemwimbia? Niliisikia siku yenu ya makumbusho na maombi, Nilishuhudia kimya, na Mbinguni mzima ikatazama kimya, Niliposikia taifa likiinuka dhidi YANGU YAHUVEH mlipokusanyika kwa maombi Kanisani, Hekaluni, Msikitini, nyumbani na mitaani, lakini ni wangapi walikuwa wanaomba kwake MUNGU wa viumbe vyote. Ni wangapi walikuwa wanaomba katika JINA la YAHUSHUA, MUNGU wenu wa Wokovu. Ole wenu. Nilimsikia kiongozi wenu akisema ombeni tu kwa mungu mnayemwabudu. Niliwaona viongozi wenu wa serikali hata wakiomba katika jina la mungu mwingine. Ambaye ni binadamu tu, shetani huja kwa mifano nyingi sana. Aibu! Ni kwa sababu ya maombi ya Watu WANGU wanaoombea huruma kwake Marekani, sikuutoa mkono WANGU wa kinga siku hiyo. Ni kwa sababu ya wale wachache katika nyumba yenu ya serikali Nilihurumia Marekani tena, katika siku hiyo, wakati maovu haya yalikuwa yanainuka, Nilisikia maombi ya watakatifu yakijaza masikio YANGU zaidi ya wale wanaojaribu kufurahisha kila dini.

Marekani, acheni kunijaribu MIMI. Ole wake mtoto anayetingisha ngumi zake kwenye uso wa Mwenyezi MUNGU YAHUVEH Anayeishi, hakuna mwingine. “MIMI NIKO” Ndiye “MIMI NIKO” na hakuna MUNGU mwingine. Marekani, msipoacha kupeperusha hiyo bendera nyekundu, nyeupe na samawati kwenye uso wa “MIMI NIKO” na mwanze kuishi maisha Matakatifu, mkiinua Bibilia, mkitii Torah, ambayo ni msimamo Mtakatifu dhidi ya maovu ya dunia hii, kama vilevile maovu yajayo dhidi ya taifa lenu. “MIMI NIKO” Atauachilia mkono WAKE juu yenu na kumruhusu shetani kuwachapa, ambapo machozi hayatakwisha, wala mayowe ya taifa hili, yatakayosikika kote duniani. Taifa la kishetani litawachapa na kuyafanya miili yenu kukaa ni kama mlichapwa kwa rangi ya nyekundu, nyeupe na samawati.

Nitamruhusu shetani kuwatia majeraha, msipokomesha kiburi chenu. Tabia hii, kuwa taifa hili ni sawa na halijaumiza yeyote au kufanya lolote baya. Kiburi chenu kinafikisha harufu mbaya hadi Mbinguni na mnanifanya MIMI kuhisi aibu, Jehanamu mzima wakifurahia na mnamfanya shetani kunikejeli MIMI akinikumbusha MIMI vile neema na Baraka ZANGU zilivyomwagwa pale Marekani. Kwa kuyafanya haya jihadharini kwa kuwa mkiendelea vivi hivi, mtalipa gharama sawa kama Babiloni, na hamtainuka tena. Kwa kweli Babiloni itaanguka lakini si kwa sasa. Shetani yuataka kuenda mbele ya wakati WANGU na Ninangoja toba ya kweli Marekani.

Taifa lenu halifai kupendelea bendera ya kitambaa cha rangi, kwa kuwa ilitengenezwa na mikono ya adui wenu, wanaotaka kukuangamiza, na ilishonwa na mikono ya adui wenu. Kwa kuwa taifa lingine linapotengeneza bendera zenu, kuzishona, hamjui ya kwamba wameweka laana zao kwenye bendera yenu, na yote inayosimamia, na wanaomba miungu yao Marekani iangamizwe. O Marekani, Nina huzuni sana kwa taifa hili, mtoto WANGU mchanga. Mmeharibika, Nimewapa baraka nyingi? Kwa kweli Nimewabariki mahali ambapo dunia inaona wivu. O Marekani, Niliwapa mengi kushinda wengine, na mnajifanya kama mtoto aliyeharibika kwa kutaka mengi zaidi, na kuniuliza MIMI kutarajia madogo kutoka kwenu. Tubuni kabla wakati haujaisha. Rudini KWANGU; msiahidi kutii bendera tu, ahidi kumtii MUNGU wenu wa Uumbaji na Wokovu, YAHUVEH, YAHUSHUA ndio MAJINA YETU.

O Marekani, Ninaomboleza na kupiga mayowe juu yenu. Ninawatuma kwa mataifa mengine na Injili ya Mwana WANGU YAHUSHUA na nchi yenu inanigeuka MIMI, lakini sio wakati wa taabu. Kwani lazima Niuondoe mkono WANGU wa kinga juu yenu ili mnisikie? Je, mwafikiria kuwa Ninafurahia kuwaona mkiteseka mbele ya macho ya dunia? Je, sikusema kupitia huyu Binti, “Marekani Nimeacha mabaya zaidi kwa yule wa mwisho, kwenu nyinyi?” Hamjui kuwa ni nyinyi wenyewe mlio na uamuzi wa hatima yenu? Marekani ilipofungua milango na kuruhusu kila dini kuja kwenye pwani zao, mnafikiria kuwa Nilikuwa Ninataka mkaribishe miungu yote ambayo wageni waliyaleta? Mmesahau haraka sana urithi wenu na mlivyozaliwa? Mmesahau haraka sana miujiza Niliyoyafanya kuzaa taifa hili?

O Marekani, msiachilie virahisi sana uhuru wenu, Niliowapa. O Marekani, msisahau kwa urahisi sana kuwa kuna MUNGU mmoja tu na ni ‘MIMI NIKO’ Ninaowafunika na kuwalinda. ‘MIMI NIKO’ Ndiye Muumbaji yuleyule Aliyewaumba kwa sababu ZANGU. Ninawatumia kujaribu mataifa yale mengine ya dunia hii. Je, watafuata njia zenu za dhambi, na ndio mtoto WANGU mchanga Marekani, mna njia za dhambi, na kwa sababu ya mfano wenu mmejaza dunia hii na mfano wa maovu. Mnawatuma wainjilisti na ujumbe wa Wokovu, na bado ni wangapi katika nchi yenu wanaoila tunda la laana, la dhambi bila kutubu. Mnayaita yaliyo Takatifu, maovu, kukufuru katika macho YANGU.

O Marekani, Njooni tukubaliane kwa amani. Mnaimba ‘MUNGU Bariki Marekani’, lakini mnajua ya kwamba wafuasi wa Buddha husema, ‘Huyu ni mungu wao mnayemwimbia kule Marekani kwa wimbo huo,” kama vile Waislamu husema, “Huyo ni mungu wao” na watumwa wa shetani husema, ‘Huyo ni mungu wao.” TAJENI ni MUNGU yupi mnaomwabudu na TAJA JINA la yule pekee Aliye Muumbaji wako, na Mwokozi wako! TAJA JINA YAHUVEH na YAHUSHUA MASHIACH pia Anayeitwa na wengine YESU KRISTO. HAYA NDIYO majina YETU na yanafaa kuwa kila mahali hewani. Kwani mwaona aibu kumwita YAHUVEH hadi mmezuia JINA LANGU kwa mashule, hadi kortini zenu? Mbona majina mengine yanapatikana pale Marekani, hata wale wanaoabudu miungu mingine?

Wageni waliokuja hapa Marekani, na bado hawaoni aibu kutaja majina ambayo ni ya binadamu tu, shetani aliyejificha, na bado yanaitwa miungu. Na nyinyi ambao mmetengwa kwa Utukufu WANGU mnaona aibu kutaja JINA lililo juu ya MAJINA yote. Alafu mnathubutu kunililia MIMI kwa huruma Marekani. O kama haingekuwa maombi ya kuomboleza ya Watoto WANGU wa kweli Ningekuwa Nimeruhusu Marekani kuondolewa kutoka kwa dunia hii. Kwa niaba ya Watoto, Bibi Arusi, Waliochaguliwa na Wateule, katika Marekani na pia wale wanaowalilia katika mataifa mengine, Ningekuwa Nimewaondoa kutoka kwa mawazo YANGU. Hivi ndivyo mlivyonikasirisha MIMI na hata kama Nimekasirika bado Ninawalilia nyinyi, na kuwauliza mtubu, kwa kuwa sitaki yeyote aangamie na kuenda mahali ambapo hapakutengenezewa binadamu, lakini kwa shetani na pepo. Ilitengenezwa kwa malaika waovu.

Marekani, Ndio Nimeuweka mkono WANGU wa kinga kwenu. Mwaona kinachotendeka Ninapoondoa mkono WANGU? Mwaona vile taifa hili

linavamiwa kwa haraka na wengine ambao wana wivu kwa Baraka Nilizowapa Marekani. Kwa kweli Marekani hamna marafiki. Wote ni maadui waliojificha na kama wangeweza wangechukua chote ulicho nacho. ‘MIMI NIKO’ Ndiye rafiki wako wa kweli na ‘MIMI NIKO’ ni Muumba wako na Baba. Mbona unaona aibu kuwa ‘MIMI NIKO’ ni nani na ni nini ‘MIMI NIKO’ Anachosimamia na hii ni Utakatifu, na yale ambayo ‘MIMI NIKO’ Ninasimama dhidi yake, haya ni maovu. Tubuni Marekani kabla muda hujaisha. O Marekani, mchanga na mjinga. Je, mwafikiria kuwa MIMI Ninafurahishwa na maombi kwa miungu mingine ambayo ni binadamu tu na shetani aliyejificha? Siku yenu ya maombi na makumbusho ilifanya kidogo sana kuniheshimu MIMI; Nililinda nchi yenu tena kwa sababu ya maombi ya watakatifu yanayofaa sana. Mnajua kuwa shetani aliuliza ruhusa KWANGU kuwaangamiza siku hiyo? Nilikataa kwa sababu maombi ya watakatifu yanafaa sana.

Jihadharini Marekani, kwa kuwa Vita vya Dunia vya 3 vijavyo vitakuwa mwanzo wa mwisho wenu na mataifa mengine pia yataanguka kama inavyokuwa kwa mchezo wa dominoes kwa laini, kama nyumba ya karata. Jihadharini na mfikirie sana juu ya haya, kwa kuwa Ninawezaje kuwabariki kushinda vita wakati taifa hili halisimamii utakatifu. Nyinyi viongozi mnajishughulisha na kuwafurahisha watu wote badala ya kumfurahisha na kumwogopa MUNGU wa Wokovu. JINA la Mwana WANGU ni YAHUSHUA na kama mnamwita kwa JINA lake takatifu au jina linalotumika sana kule Marekani liitwalo Yesu, yeye ni Masihi yuleyule milele na hakuna mwingine. YAHUSHUA Ndiye njia ya pekee kuja kwa ‘MIMI NIKO’, hakuna MUNGU mwingine ila Utatu Mkuu kwa kuwa sote watatu ni moja.

Jihadharini, kwa masihi wengi bandia wanaoinuka kote. Jihadharini, yote yaliyo kwenye Bibilia shetani yuataka kukopi. Jihadharini kwa kuwa Watoto, Bibi Arusi, Waliochaguliwa na Wateule WANGU, watadanganywa iwezekanavyo. Kwa kuwa shetani yuaja kama malaika wa nuru, na hujifanya ni kwa faida yako, kukulinda, na bado mjihadhari kwa kuwa mtakapomkimbilia yeyote kukulinda kwanza kabla ya kumkimbilia YAHUVEH na Mwana WANGU YAHUSHUA, mmeanguka katika mtego wa kudanganywa na uongo. Jihadharini Ninaposema kwa wale ambao YAHUSHUA amewaokoa kuwa wameokolewa kwa kweli alafu nguvu za dunia hii zije kuchukua uhuru wenu wa kuongea, kusafiri, hata vile mbegu zenu zitapandwa mbali nanyi. Jihadharini kwa kuwa hawa waovu watajaribu hata kupima mnachokula, kunywa na kuvaa na SIKU IPI MTAKAPOABUDU!

Siku zote mnafaa kuniabudu MIMI, lakini kuna Sabato moja tu ya Kweli na hiyo ndiyo siku YAHUSHUA Alitupa Akituonyesha mfano na akawa Bwana wa Sabato. Niabudu na kunisifu YAHUVEH na YAHUSHUA kila siku, lakini sanasana kwenye siku ya Kweli ya Sabato ya Kiebrania pumzikeni katika YAHUVEH kwa kuwa Nilipumzika baada ya kuumba dunia hii. Wewe ni nani, binadamu tu kufikiria kuwa hauhitaji kupumzika. Fuateni Torah YANGU. Heshimu siku ya Kweli ya Sabato na iwe Takatifu mbele YANGU. Pumzikeni katika siku hii. Tafuteni kusikia kutoka KWANGU katika siku hii, Niulize MIMI kuwa Nataka mfanye nini katika siku hii, jitenge kutoka kwa dunia na kuheshimu MUNGU wa viumbe vyote na Wokovu. Je, binadamu atamwibia MUNGU? Ndio, hata siku za Kweli za Sabato zilizotengwa kwenu na ‘MIMI NIKO’ kwa kuwa haya yatakuwa ya sasa na milele, siku ya pumziko.

Tazameni siku ambayo dunia husherehekea, na ipo katika ulevi, dhambi, imeenea kote na jueni haya ni uongo wa shetani kunikasirisha ‘MIMI NIKO’ kwa kuwa wengi hawaelewi ni siku ipi ni Sabato ya Kweli. Someni maandiko yenu, si Neno LANGU lasema, “Fanyeni kazi siku 6 alafu katika siku ya saba pumzikeni?” Hii si sheria tu, hii ni Baraka iliyowekwa kwenu na kwa ‘MIMI NIKO’. YAHUSHUA Atawarudia Bibi Arusi WAKE katika siku ya Kweli ya Sabato lakini hamjui ni Sabato ipi atarudi, kwa hivyo jitayarisheni. Asiwapate kama mnakunywa, kusherehekea, na kufanya kazi, kama dunia inavyofanya kazi au utalia kama wale bikira 5 wajinga wasio na mafuta katika taa zao. Washeni taa zenu sasa na mziache kama zinamulika, mpaka mtakapomwona YAHUSHUA akirudi katika Utukufu WAKE kwa Bibi Arusi WAKE wanaomngoja Bwana Arusi wao.

Jihadharini kwa kuwa minara ya Kituo cha Biashara Duniani (WTC) imefananishwa na Nguzo ambazo Samsoni alitingiza. Marekani hapa ndipo mnapoweka imani yenu, tumaini lenu, hizi ni minara ambayo ilitengenezwa na lugha tofauti na mataifa, na mkajenga mnara huu, na kama mngeweza mngekuwa mmefikia urefu wa mnara wa Babeli. Kama vile mnara wa Babeli ulivyoanguka mbele ya dunia, Niliruhusu minara hii kugongwa chini. Sasa ardhi hii imelowa damu ya walioaga ambao wapo chini ya mnara huo kama kumbusho kwa dhambi ya kiburi katika minara hiyo. Hakuna yeyote anayezungumzia dhambi zilizokuwa ndani ya minara hii, dhambi ambazo dunia mzima iliabudu, dhambi ya ulafi, wizi, pesa za damu, katika mifano nyingi, dhambi katika mifano nyingi zisizowezwa kutajwa. Dunia mzima ilikunywa kutoka kwa kikombe hicho cha Babeli, Nilipoachilia mkono WANGU juu yenu siku hiyo; adui aliingia na kuwavamia.

Dunia ilitazama kwa hofu, walipoona minara ya kituo cha biashara duniani (WTC) yenu ikiwaka moto na kuanguka chini. Nina huruma kwa mfumo wenu wa kifedha kwa sababu moja tu. Msifikirie ni kwa sababu Marekani wana nguvu sana, kuwa hakuna yeyote anayeweza kuwaletea shida tena kwa kuwa ni maombi ya watakatifu katika JINA la Mwana WANGU sijaruhusu uchumi wenu kuanguka chini. Bado! Kama tu maombi yataendelea kuja juu na imani kwa ‘MIMI NIKO’ zaidi ya serikali hii na serikali nyingine.

Marekani, fikirieni sana kabla hamjajihusisha katika vita vingine. Je, ni taifa gani mtakalopigana nayo? Hamna taifa lolote kupigana nalo. Nyinyi ni wadogo sana kushinda mataifa mengine makubwa. Nyinyi ni kama mtoto mchanga anayejaribu kushindana na yule mkubwa. Sababu pekee iliyosababisha mshinde vita hapo awali ilikuwa kwa sababu wengi katika taifa hili walikuwa wamemkaribia ‘MIMI NIKO’ na Mwana WANGU YAHUSHUA na mlijua kuwa bila SISI kwenye upande wenu mngekuwa mmeshindwa katika kila vita. Hata jina lenu mlipewa na ‘MIMI NIKO’. (US), YAHUVEH na YAHUSHUA ndiyo (US) SISI na A inasimamia (Almighty) Mwenyezi. Taifa hili lilifaa kusimamia Muungano wa Mataifa ya Mwenyezi. Kwa kuwa hapo awali mlikuwa mnamtumikia MUNGU Mwenyezi Anayeishi ‘MIMI NIKO’ na YAHUSHUA. Ilikuwa ni kwa neema, upendo, huruma na hekima ya ‘MIMI NIKO’ Niliwapa viongozi wenu wa siasa na kiroho.

Ni nani atakayesikiza sasa? Ni roho ipi inayozungumza kupitia viongozi wenu? Waombeeni. Ikulu yenu imechafuliwa na haijasafishwa kutoa pepo za uchawi, uzinzi, mauji, kujiua, ukahaba, usherati, ulafi, wivu, mpinga kristo, kuavya mimba, ushoga, kiburi, kukataa mungu, kukosa upendo, chuki, kunyimana, hongo, pepo za uongo na udanganyifu, ushetani, wazimu, upatanisho, kuzungumza na walioaga, Nahitaji kuendelea? Ni roho ipi iliyoko kwenye Ikulu sasa ambapo viongozi wenu wanafanya maamuzi? Je, Damu ya YAHUSHUA inayopaswa kusafisha nyumba zenu za serikali ipo wapi? Je, kutubu kuko wapi kama Niliyoiulizia pale Washington DC? Kutoka kwa viongozi wenu waliohusika kupitisha amri za maovu? Watu wanasimama kati kwa viongozi wenu wa siasa kote duniani.

Marekani, msiende vitani, bila ‘MIMI NIKO’ kando yenu. Msiwaache wanasiasa wenu kufikiria kuwa mnataka vita hivi na adui asiyeonekana. Je, mnaweza kupigana na mataifa 60 au zaidi kuwapata wanaume mnaowaita magaidi? Je, mnawezaje kufikiria kuwa mtashinda? O Marekani, mnasimama mbele ya dunia iliyojaa na maadui wanaotaka sana kujifanya kama rafiki na kwa kweli watakusaliti ukiwapa nafasi. Watakuvamia wakati usipotarajia. Mnawapa mkono uliojaa na pesa, na hongo, na wanakuchukia kwa sababu ya haya. Mmeonywa! Marekani, mpo karibu na moyo WANGU, kwa kuwa hata kama adui wenu wana kiu na njaa mwataka kuwalisha na kuwapa maji. Je, hamjui ya kwamba kuwa mnawapa maadui wenu nguvu badala ya kuwapunguza nguvu? Mnaweka makaa ya moto kwenye vichwa ambavyo havitambui MUNGU wa baba zenu wa kale, wanakuchukia mnapowaonyesha upendo na huruma, na wanakuangalia ni kama wewe ni mnyonge na sio mwenye nguvu. Marekani hata baada ya vita na maadui mnarudi kwao kujenga nchi yao lakini hamwezi kufuta machozi mliyosababisha kwa sababu mko na haraka sana ya kuonyesha wengine mnayofikiria ni mikono ya nguvu, misuli yenu, na kumbe wakati misuli yenu haina nguvu ya Neno Takatifu la YAHUVEH mtapata kuwa itakuwa vigumu sana kufanya kama hapo awali.

Jihadharini, mkono wa adui, msiwaamini maadui wenu. Jihadharini kwa kugeuza mgongo wenu kwa adui kwa sababu sasa kuna zaidi ya taifa moja na adui ambao mnafaa kuwachunga. Nilimwonya huyu Binti Ninayezungumza kupitia kwake, JIHADHARINI NA PAKISTANI na ni wangapi wanaozungumza na kuonya viongozi kuhusu taifa hili? Marekani, mnatabasamu na mataifa mnayofikiria yanatabasamu pia yanashika silaha nyuma yao. Vita vitawaumiza kwa njia ambazo hazifanyika bado. Njia ya pekee itakayofanya haya yasifanyike ni maombi ya watakatifu ikiendelea kumwita RUACH ha KODESH (ROHO MTAKATIFU) WANGU Afunike Marekani na watubu na kusimama katika Utakatifu na ujasiri, kemea maovu na msiite JINA lingine ila tu YAHUVEH na YAHUSHUA. Funikeni Rais wenu Bush katika maombi, na ole wenu wakati rais wenu afuatayo atakapokuja. Ole wenu wakati Papa afuatayo atakapokuja. Kwa kuwa huyu Papa afuatayo hatakuwa mtu wa amani, na atatumiwa na shetani.

Kumbukeni Ufalme wa Warumi na walichofanya. Maneno kwa wenye hekima katika YAHUVEH, ombeni sasa, kwa nyakati zijazo, zitawajia haraka sana kwa kuwa wakati huu ndio wakati wa kurekebisha vitu NAMI, Ninazungumza haya kwa dunia mzima, kwa kuwa Marekani, mnaweza kuwa mfano, kama vilevile Israeli, kama tu watoto WANGU wawili watasikiliza, basi dunia hii haitalazimishwa kunywa kikombe cha ghadhabu ZANGU. Ah, lakini ilishasemwa na tayari kukadiriwa, lakini msikimbize wakati WANGU. Kuna wakati bado kama nyinyi mnaosema mnamjua ‘MIMI NIKO’ hamtanyamaza kamwe. Vita hivi vya Dunia vinaweza kucheleweshwa zaidi; hakutakuwa na vingine kama hivi, baada ya haya kutakuwa na vita dhidi ya Mbinguni yenyewe. Ombeni kuwa mtakuwa katika upande wa Mbinguni na sio upande wa mpinga kristo.

Sasa kwa kufunga, Ninataka kuwabembeleza Watoto WANGU wanaokuja KWANGU na machozi, na wanaogopa yatakayotendeka. Kama maneno haya ya hekima hayatasikizwa, ‘MIMi NIKO’ hakuwapa roho ya kuogopa, lakini ya nguvu, upendo na akili timamu. Nipe asante MIMI kabla ya wakati wa Miili yenu ya Utukufu. Miili ambayo chuma zozote hazitaweza kuwazuia, miili ambayo haiwezi kuuliwa, miili itakayofanya yale ambayo watakatifu walifanya wakati Mwana WANGU YAHUSHUA alifufuka kutoka kaburini. Watakatifu walifufuka pia Yerusalemu Roho zao zilipokuwa zinaunganishwa na miili yao na wakafufuka katika miili yao ya kufufuka, kuwa shahidi YAHUSHUA aishi, aongoza na kutawala. Tena, Ninasema ilivyokuwa hapo awali ndivyo itakavyokuwa tena.

YAHUSHUA alikuja kwanza alafu watakatifu wakafufuka na kushuhudia kwa wote Yerusalemu. Someni Neno LANGU Takatifu, kama ilivyokuwa hapo awali ndivyo itakavyokuwa tena. Hawa ndio wale waliokufa katika MASIHI ambao watahubiria wote duniani; YAHUSHUA ni MASIHI, pamoja na wale ambao wako hai na kuitwa Bibi Arusi WANGU. Wakitazama, wakingoja, lakini wakifanya kazi zao waliopewa na Baba Aliye Mbinguni, watanyakuliwa kukutana naye YAHUSHUA angani. Hamna tena miili ya nyama na damu, lakini tu Miili ya Utukufu, yatakayofanya mengi kwake ‘MIMI NIKO’ kuliko miili ya udongo.

Kama mnaamini Neno LANGU Takatifu basi mnajua kuwa hii sio mara ya kwanza ‘MIMI NIKO’ Ameyafanya haya, kumbukeni Eliyah wa kale, kumbukeni Enoki? Mbona mnafikiria kuwa Naweza kuyafanya haya mara mbili tu, je, ‘MIMI NIKO’ hawezi kuyafanya haya tena na kwa wale wanaoniamini kwa imani Nitayafanya. Wakati watoto wa Israeli walikuwa karibu na watoto wa Misri, na bado mapigo hayakuja karibu nao, hata giza haikuwaangukia. Damu ya mwanakondoo aliyechinjwa ilikuwa juu kwenye milango, sasa mna Mwanakondoo mwingine Aliyechinjwa, Mwanakondoo Mtakatifu wa pekee Aliye bila doa wala waa. Hakuna dhambi yoyote iliyopatikana ndani ya YAHUSHUA. Kwa hivyo wale ambao wameosha Hekalu zao zinazoishi katika Damu YAKE iliyomwagwa pale Kalvari, kwa msamaha wa dhambi zao, kutubu na kuepukana na dhambi, wanaompenda na kumtafuta YAHUVEH na YAHUSHUA wakiwa kwanza kwa maisha yao, waliojawa na RUACH ha KODESH WANGU.

Kama ilivyokuwa katika nyakati za Farao Mwovu, wakati pepo ya farao mwovu itarudi tena, basi pia miujiza itarudi tena, kama Musa na watoto wa Israeli. Kama mnaweza kuamini, basi miujiza yasiyoweza kuelezwa mtayaona. Bado Nitakuwa na watakaouawa kwa kuwa ishakadiriwa na wanajua katika roho zao na wako tayari, lakini Watoto WANGU wanaoweka imani yao kwangu ‘MIMI NIKO’ na husikiza sauti YANGU, watajua ya kufanya, na wapi pa kuenda, na wataepuka mkono wa adui kila wakati. Sio wote watakaopata Miili ya Utukufu, kwa kuwa sio wote wanaoamini. Wengine wanataka kunijaribu MIMI na kubaki na wapendwa wao ambao hawajaokoka. Kueni na imani kwa miujiza inayotakikana, kujaribu na kuwaonya wasikubali Alama ya Mnyama, wengine wanajua kuwa watapata Miili ya Utukufu, hii ndiyo sababu kuna mgawanyiko, wote wako sawa. Tayari Nishaiweka katika roho zenu kama wewe ni WANGU, kama mtakuwa watakaouawa, au kama mtakuwa mmojawapo ya wale waliokufa katika MASIHI, na mtakufa kwanza, kufufuka, au kama mtanyakuliwa na kukutana NAMI angani kama bado mpo hai.

Acheni vita hivi vya ujinga. Hamwezi kuona kuwa hii ndiyo sababu Nilizungumza kwa huyu Binti Sherrie Elijah na kusema, “Kunyakuliwa kwa kwanza alafu kwingine kwa wale Niwapendao?” Ninawapenda wote! Waliokufa katika MASIHI na kufufuka, na nyinyi ambao mko hai kunyakuliwa kukutana NAMI angani. Bado hamwoni, hii ndiyo sababu Nilizungumza kwake, na kusema, “Msiseme pre-trib, mid-trib, au post-trib, kwa kuwa sio yoyote kati ya hizi vitu. Hamwoni ni kwa sababu nyote mko sawa. Hata wale wanaoamini YAHUSHUA atakuja tena baada ya Dhiki Kuu, kwa kuwa si YEYE yuaja kuongoza na kutawala hapa duniani kama Anavyofanya Mbinguni? Mmenikera MIMI sana kuhusu mgawanyiko huu wa ujinga. Je, sasa mnaweza kuusahau mjadala huu? Chuki kuu na hisia mbaya kutoka kwa watoto WANGU imesababishwa na mjadala huu ambao shetani ameuanza ndani yenu. Fanyeni kazi pamoja, sio kila mtu kivyake. Acheni kuwakataa Mitume na Manabii WANGU. Mwahitaji macho na masikio ya mwili wa YAHUSHUA. Wachungaji, acheni kufukiria kuwa kundi hawahitaji yeyote isipokuwa wewe tu. Kundi sio wako lakini wao ni wa Mchungaji Bora. Imetosha.

Mtasema nini kwa wale watakaoachwa nyuma, kwa sababu mlikataa kuwaruhusu Manabii na Mitume wangu kuwaonya kondoo na Wanakondoo na kondoo weusi ambao wangekuwa weupe, lakini mlikuwa mwajaza mifuko yenu na dhahabu, na hamjali ambapo kondoo na wanakondoo wanapotea, heri tu wasiwaite kutubu. Kondoo na wanakondoo wanakula chakula kilekile kila siku. Mnaogopa wengine kuwalisha, mkiogopa, shirika Niitalo Kondoo na wanakondoo WANGU, watataka chakula cha roho kutoka Mbinguni, mvinyo mpya na kusisitiza kuwa wachungaji, watupe mvinyo wa kale ili kibuyu cha mvinyo usipasuke.

Wachungaji, mtawajibika kwa kila nafsi mliopoteza katika shirika lenu na anayekosa kuenda Mbinguni kwa sababu ulikuwa unajijali wewe mwenyewe, na kujenga ufalme wenu wa kiroho, na sifa zenu, mkiyageuza Maandiko YANGU kufanana nanyi, kueleza utajiri wenu. Na Watoto WANGU hawana chochote, mnapojijaza na kiburi, mkitajirika kwa kukosa kuongea ukweli mkiogopa itawakera kondoo na wanakondoo. Wewe ni maskini kule Mbinguni. Mnavaa suti zenu na kuishi katika majumba makubwa hapa duniani, kwa kweli haya tu ndiyo mtakayokuwa nayo hapa duniani, Mbinguni hamna chochote, haijalishi kama mnahubiri vizuri sana, na kufunza, tuzo ZANGU sikuzichukua mlipoenda katika njia ya dunia, kwa hivyo mmewadanganya wengi, lakini sio Watoto WANGU wote kwa kuwa Nimepeana karama ya utambuzi na wanawajua kwa roho gani inayowaongoza, roho ya pesa na ulafi. Wewe ni kahaba katika macho YANGU.

Hekalu yenu ya Kioo itavunjika mnapoendelea kusimama pale katika kiburi chako na utukufu wa mwanadamu. Utukufu WANGU haupo ndani yako. Wale ambao wanataka kukuita mchungaji, siku moja wataona Hekalu yako ya glasi ikivunjika, Nikiitingiza, na wote walio ndani wataangamia. Ni wachache sana ambao haya yakitendekea wataona Mbinguni. Si Niliwaonya kuhusu kuwatafuta viongozi wa Kiroho ambao ni namna ya kupoza masikio yenu. Mmeonywa! Minara ya binadamu inayokejeli ‘MIMI NIKO’ itaanguka. Ndio, hata wale wanaofikiria wao wenyewe ni minara, na kujiita kwa JINA LANGU na hata hawanijui MIMI. Mtaanguka, viongozi hawa wa kiroho watakapoanguka, kondoo na wanakondoo watatoweka, ni wachache sana watakaompata Mchungaji Bora.

* * * * * * *

Imezungumzwa, imeandikwa siku hii ya Oktoba 1, 2001 Saa 12:10 Usiku. Ninatoa haya na kuuliza msamaha wa YAHUVEH kama sikuaandika yote ninayofaa kuandika. Nimefanya yote niwezavyo, na kujaribu roho inayozungumza. Tafadhali niambie kama umesikia sauti ya Baba yetu Aliye Mbinguni. Pia ninahitaji kupewa moyo wakati jumbe hizi za kinabii zinapowasumbua adui wanaotaka kunyamazisha huyu binti wa YAHUVEH na YAHUSHUA. Hata hivyo, Ninataka kumfurahisha YAHUVEH na YAHUSHUA hata kama sitaweza kuwafurahisha wanadamu. Mtume Sherrie Elijah. P.S. Msimrushie mawe mjumbe huyu.

Hiki kitambulisho ni mwanzo wa Alama ya Mnyama. Nilipokuwa nimelala niliamka na maarifa haya kutoka kwa YAHUVEH, kitambulisho ni nini? Ni Alama ambayo inakutenga kwa wengine. Je, habari hii inaenda wapi? Katika kompyuta iliyoko Ubeljiji inayoitwa “BEAST”. Jihadharini na mwanzo wa yale yaliyoandikwa katika kitabu cha ufunuo inayoitwa Alama ya Mnyama. Ombeni kuwa wote wanaoita jina la YAHUSHUA hawatakuwa hapa wakati haya yatakapotendeka. Kwa kuwa hakutakuwa na kununua wala kuuza bila Alama hii. Tony Blair anajaribu sana kuyaleta haya katika Uingereza. Watu zungumzeni au myamaze kamwe.

Barua pepe nilizopokea;

Jambo kuu ninaloona katika neno hili mpya kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni haya. Kama Wachungaji, Wainjilisti, Walimu, Manabii, Mitume, hawataacha kudanganya, na kuanza kuwaambia watu ukweli, taifa hili limekwisha. Wewe ni mwenye moyo mjasiri unaosimamia ukweli. Endelea kusimama na ninaomba wengine watafuata mfano wako wa ujasiri. Bila kanisa kusimama pamoja katika toba ya kweli, na kumlilia Mungu kutusamehea kupuuza kwetu na dunia, mwili, na shetani, sisi tumekwisha.

Jambo hili linategemea kanisa zote wanaosema wanajua Mungu wa kweli na Neno Lake Takatifu. Nilitazama TBN na kumwona Paul na Jan Crouch. Alikuwa anashika Korani katika mikono yake akiwaambia mamilioni ya Wakristo Marekani vile Waislamu walivyo na amani na upendo na Mohammad alikuwa mtu mzuri. Hii ilikuwa wiki mbili iliyopita kabla ya Minara kuvamiwa. Hii ni mfano wa ujinga ambao wachungaji na wahubiri hawa wa leo wamejawa nao. Ninaona wamejifunika kwa mafunzo ya uongo na kupuuza ukweli. Niliona siku hii ikija miaka 12 iliyopita, na nikajaribu kuwaambia wengine… hakuna yeyote aliyesikia. Sasa unaambia dunia kupitia intaneti. Naomba wawe makini na kusikiza, alafu watende ipasavyo au tumekwisha!!! “Kupuuza ukweli, O kupuuza ukweli imefanya Kanisa LANGU kujipata katika mambo haya, Asema Bwana MUNGU. Kimbieni kutoka kwa huu kupuuza ukweli au mtakamatwa katika uchafu huu wa dunia hii na kufunikwa kwa maovu haya, Asema Bwana MUNGU”.

Asante Sherrie kwa kusimama imara katika ukweli wa MUNGU. Ninahisi kukuambia uweke ujumbe huu karibu na Unabi huu kwa tovuti yako. Itaambatana na maneno mazito ya Mwenyezi Mungu, MIMI NIKO Mkuu Aliyokupa. Tunatoa sifa na asante, na tunatoa heshima na utukufu unaostahili kwake Mungu Baba, Roho Mtakatifu, na Yahushua, Mungu na MWOKOZI wetu. Itawaamsha wengine kwa yale yanaoyoendelea katika dunia ya kanisa, lakini tumia busara yako mwenyewe.

Upendo, Linda.

* * * * * * *

Dada Sherrie, Nimesoma ujumbe wa #54 na Nikahisi Roho Mtakatifu katika kila neno. Kila neno lililo na Baraka na upako lilisema “Ukweli” katika nafsi yangu na ninamsifu Mwenyezi Mungu kwa kutufunulia moyo Wake kwetu sisi! Ninaomba pia kuwa wote watakaosoma ujumbe huu watasikiza, na nitafanya juhudi langu kwa kunakili haya na kusambaza ujumbe huu kwa marafiki na wapendwa wangu. Ninaona shida zangu mwenyewe, lakini ninahuzunika sana kwa vile watu walivyosahau Mungu katika jina la “kupuuza ukweli” na wamekataa kutumia jina la pekee linaloweza kutuokoa “YAHUSHUA”! Unabii huu ni kiamsho kikuu kwa Marekani na dunia na ninakubaliana nawe pale uliposema kuwa kila mtu alikuwa akiruka akisema “Mungu Bariki Marekani”. Mungu awezaje kutubariki sisi katika dhambi, uasi na kiburi! Kwa kweli! Toba na uvumilivu ndio kinachotakikana na ninaombea nafsi zote kurudi kwa Mungu wa pekee na wa kweli Anayeishi, YAHUVEH! Asante Dada kwa kuwa chombo ambacho unabii huu umekuja kutuonya kabla wakati haujakwisha. Mungu akubarki kamwe!

Olga

* * * * * * *