UNABII WA 1
HUKUMU HUANZA KATIKA NYUMBA YA YAHUVEH!
Alipewa Rev. Sherrie Elijah Disemba 31, 1996.
* * * * * * *
Ni jambo la kuogopa na kutisha kuanguka kwenye mikono ya MUNGU aliye
hai. Ghadhabu YANGU yaweza kuwa kuu
Lakini wao hufikiria MIMI NI kipofu na kiziwi. Mwaka wa 1997,
Nitawaonyesha kuwa MIMI ni MUNGU wa moto na kitakachosimama njiani mwa Wahubiri
WANGU kitachomwa kwa hasira YANGU. Wale ambao huthubutu kukomesha INJILI ya
YAHUSHUA ha MASHIACH watateseka zaidi. Ninaijia kanisa isiyo na doa wala
kunyazi na tena Nawaambia, wape onyo kanisa. Kanisa si Mchungaji, si mjengo.
Kanisa ni watu, Kondoo WANGU. Nimechoshwa na binadamu kuziita huduma kwa majina
Kama wana dhambi na wao si kamili, hawana haki yoyote kuita huduma kwa
majina
Tena, Natabiri kupitia kwako na kusema jihadharini. Wape onyo, kwa kuwa
binadamu asiye kamili atakapoanguka (na ataanguka) huduma iliyo na jina
Lakini wape onyo, ni
Lakini watoto WANGU hawana lolote la kuogopa, wale wanaonipenda kweli,
wanaoniabudu, wanaoniweka MIMI kwanza katika maisha
Lakini, kusiwe na vita vya kiraia katika kanisa ZANGU. Kusiwe na
ubaguzi, iwe umbo la nje au kirangi. Kwa kuwa Watoto WANGU wanapoonana,
wanapaswa kuona NYEKUNDU pekee, DAMU YANGU! Acheni kugawa kanisa zenu kwa
rangi. MIMI sioni rangi yoyote. MIMI ni rangi zote katika moja. Acheni
kuhukumiana kwa umbo la nje. Kwa kuwa mahali roho ya ubaguzi ipo, RUACH ha
KODESH (Roho Mtakatifu) WANGU hatabaki, hataishi. Badala YAKE, pepo mbaya
zitaruhusiwa ndani. Mmepewa onyo.
Sherrie, (Elisabeth) haujajua ni nini utaandika kutoka neno moja hadi
lingine. Wape unabii huu wale wote walio na masikio ya kusikia, wacha wale
wengine wabaki viziwi. Ninaijia kanisa isiyo na doa wala kunyazi.
Kinachonishikilia MIMI, ni kile kinachotakikana kunirudisha MIMI. Kanisa YANGU!
Watu WANGU! Wachungaji WANGU! Wahubiri WANGU! Ninachukia kiburi! Ni moja ya
dhambi 7 hatari, lakini bado wachungaji WANGU wanaobeba upako WANGU hufikiria
wao ndio hujenga kanisa, kanisa ni zao na lazima wapate udhibiti wa kondoo.
MIMI pekee ndiye Mchungaji Bora. Kazi yenu ni kuwa kidole kitakachowaelekeza
KWANGU, YAHUSHUA.
Kiburi, kiburi kuu, imeingia katika hekalu Nilizozimwagia upako WANGU.
Ni nani aliye na mkusanyiko kubwa, pesa zaidi? Haya hunikera MIMI. Ni nani
anayeshinda roho nyingi? Wivu na tamaa ziko katika hekalu ZANGU. Haya hunikera
MIMI. Mnasema, “YAHUSHUA yuaja lini tena?” Nasema, “Nimekuwa
nikingoja kanisa, hekalu hizi, wajisafishe.” Acheni kuhojiana kati yenu
wenyewe. Fichua mbwa mwitu ambao wamekuwa wakiwala Kondoo WANGU. Wapo nyuma ya
mimbari na watu wote wanajali tu kanisa zao, hakuna yeyote anayewajali kondoo.
Nani anaweza kujenga hekalu kubwa? Nani anaweza kuwavutia zaidi
wanahabari? Ni mwinjilisti yupi, nabii yupi, mchungaji yupi, kanisa ipi, aliye
au iliyo nambari moja? Ninawaambia kupitia huyu Nabii, msikilize. Hukumu huanza
katika nyumba ya YAHUVEH! Alafu nitakabiliana na wapagani. Haya hunikera MIMI.
Nina hamu ya kuwakumbatia nyote mikononi MWANGU, na bado mnahojiana na
kutusiana kwa sababu ya jinsia yenu. MIMI huchagua kumtumia yeyote Nitakayechagua
kumtumia. Aliye mnyenyekevu kati ya wote Nitamtumia kwa njia hodari.
Nachagua kutumia chombo hili kwa sababu yeye hufikiri ya kwamba yeye
ndiye mdhaifu kati ya wote, lakini Nasema tena, Nitatumia wale wanyenyekevu na
wapole, wale ambao hakuna yeyote hufikiria kuwa naweza kuwatumia, kwa nguvu
YANGU hujitokeza bora kwa wale watu wadhaifu. Wengine hujua kuwa nguvu hii sio
RUACH ha KODESH (Roho Mtakatifu) hutumia walio tayari, vyombo vya udongo
walio watiifu, si wale wanaopiga kelele, “Nitumie mimi kwa sababu mimi ni
mrembo, mimi ni mtakatifu kushinda wote.” Sitatumia wale wanaofikiria wao
ni dhahabu; MIMI hutumia wale wanaojua wao ni vyombo vya udongo vilivyovunjika lakini
wao ni shujaa hodari wa YAHUSHUA ha MASHIACH. Katika 1997, Nitawazindua wale
walio na huduma zilizobaki katika unyenyekevu au wasiojulikana kwa umati. Wale
ambao sikuwaita tu lakini waliochaguliwa, wamechaguliwa kwa sababu ya imani
Kuwa tayari, kwa katika 1997 nawaambia
Kuwa tayari, kwa sababu kwa Watoto WANGU, huu ndio kumwagwa mkuu wa
RUACH ha KODESH (Roho Mtakatifu). Nitatumia wale wanaofikiria hawajulikani, si
warembo, hawana elimu, wale wanaojua hawawezi kufanya chochote bila upako WANGU
wa RUACH ha KODESH (Roho Mtakatifu). Wale waliotupwa, walionyanyaswa,
waliopuuzwa, walioambiwa wakate tamaa, hakuna thamani.
Wale ambao hawajakuwa na fedha watamtegemea Mwenyezi MUNGU na
nitawafungulia dirisha za mbinguni na kuwabariki zaidi hadi watalazimishwa kuwapatia
wengine ili wao pia wabarikiwe zaidi. Na hili litakuwa jambo ambalo litatendeka
mara kwa mara. Neno LANGU husema, “Mpenzi, naomba ufanikiwe katika mambo
yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.”
Nitawaonyesha ya kwamba Neno LANGU haliwezi kurudi KWANGU tupu.
Jihadharini nani unayemtupa
Jihadharini na kuwakana wainjilisti wasiojulikana katika macho yenu, na
wanaotumia fedha zao kueneza injili ya kushinda roho. Jihadharini kukejeli,
kuwatusi na kudharau Nabii anayekuja kwako na unabii na kwa sababu hautaki
kuamini unabii huo kwa sababu wao ni jinsia tofauti au hawajulikani na wao sio
maarufu. Jihadharini kuwakosea watoto wadogo Ninaowatayarisha kutabiri na ndio,
kuwapa onyo wazee wasikilize sauti ya Mwenyezi MUNGU.
Tokeni katika kiburi. Kwa sababu hawa ndio Ninaowatuma. Mkiwakosea,
mnamkosea MUNGU aliyewatuma. Wao ni Wajumbe WANGU, kwa hivyo msimpige mawe
mjumbe. Ni hawa wasiojulikana Ninaowainua, kupitia wasiojulikana Nitawatumia
kufanya ishara, maajabu na miujiza YANGU, na kwa kuwa mdomo wa YAHUVEH. Kwa
kuwa hao sio wasiojulikana.
Hamkujenga hizi huduma zilizofanikiwa. Ilikuwa kwenye nguvu na upako wa
RUACH ha KODESH fanaka ilikotoka. Acheni kuchukua Utukufu WANGU. Wewe sio
mponyaji, mkombozi; ni Mwenyezi YAHUVEH pekee anayekomboa. Ujumbe kwa kanisa ya
1997 ni kuwa mnyenyekevu mbele ya YAHUVEH. Huu ujumbe ni wa Manabii,
Wainjilisti na Wachungaji. Hamna nguvu yoyote bila upako WANGU. MIMI ni MUNGU
aliye na wivu. Toa jina ya binadamu kutoka kwa huduma ZANGU. Mmepewa onyo. Pea
sifa, utambuzi kwa yule pekee aliye na haki kuita huduma kwa jina lake, Bwana
na Mwokozi wako, yule unayetangaza kumtumikia na kumwabudu. Mimi huwa sishiriki
Utukufu WANGU na binadamu yeyote.
Kuna funzo la uongo linaloenezwa katika nyakati hizi za mwisho kwenye
kanisa ZANGU ambapo upako WANGU umemwagwa. Roho ya kiburi na dini imeeneza
uongo ambao wachungaji wanasema ni ‘Sisi’ pekee tulio na mamlaka ya
kusema ni nani anaweza kuomba na nani hawezi kuomba. Mmekatazwa kuombeana bila
ruhusa. Hata Mwenyezi YAHUVEH, Muumbaji wa Mbinguni na dunia hawezi kunena jambo
kama
Neno LANGU linasema wazi, “Mwombeane.” Mimi sina upendeleo.
Kwa hivyo, kwa nini ningeruhusu jambo
RUACH ha KODESH anaweza kabisa kuwalinda wale wanaoombewa. Acheni
kujaribu kufanya kile ambacho hamtakikani kufanya. Hii ni kazi ya RUACH ha
KODESH. Hii ni kazi ya Mchungaji Bora na MIMI pekee ndiye Mchungaji Bora;
Ninaweza kuwalinda wote walio WANGU. Toa boriti machoni mwako kabla hujahukumu
kuwa mtu fulani hafai kumwombea mwingine. Hukumu huanza katika nyumba ya
YAHUVEH. Nitafanya usafishaji kwa njia hodari katika 1997, kabla sijawahukumu
wapagani. Dhambi ni dhambi. Ukosefu wa utakatifu bado ni kutokuwa na utakatifu.
MIMI sio MUNGU anayebadilika na nyakati ZENU. MIMI niko sawa jana, leo na
milele.
Kwa sababu wachungaji wanakataa kuwa na ujasiri wa kusimama na kusema
tubu na neno la YAHUVEH husema hii ni dhambi. Wanaogopa kupoteza hali ya
msamaha wa kodi, na huruhusu serikali kuwanyamazisha kwa sababu ya kuogopa.
Sasa watakuwa na mtu wa kuogopa, MIMI YAHUSHUA. Kwa sababu mlibaki kimya, na
hamkuzungumza na kusema tubu au moto wa Jehanamu utakuchoma. Kitu kimoja
ambacho nyinyi wachungaji na wahubiri mliogopa kitawapata ghafla. Hamtakuwa na
hali ya msamaha wa kodi. Nitairuhusu serikali kuichukua tena ndio mtazungumza
bila kuogopa, kuwa dhambi ni nini. Hili litakuwa ishara ya kwamba unabii huu
umetoka KWANGU kwa kuwa mtaliona jambo hili likija kutendeka. Kukuza haitoki
kwingine ila pale kaskazini ambapo ni Mbinguni.
Ni MIMI ninayemkuza mmoja na kumwondoa mwingine. Wengi wataondolewa
katika 1997 waliotengeneza faida wakiuza zawadi za RUACH ha KODESH. Hazikuwa
zenu kuuza. Wale waliongia katika huduma hii na kufikiria kwamba hii ni njia ya
kupata
Wachungaji, Wainjilisti, manabii, Wahubiri, Watoto WANGU…
mtawajibika kwa yale yote mnayoyajua. Kadhaa wanajua mengi zaidi ya wengine,
lakini wanawajibika zaidi kwa sababu wanajua bora kuliko kunikosea MIMI. Katika
1997 tafuteni ndani yenu wenyewe na kutojali maisha ya uovu na roho za kiburi
na uasi. Kwa sababu MIMI ni MUNGU anayejua, huona na husikia yote. Wale
wanaojiita Kondoo WANGU na wahubiri watawajibika kwa yale yote wanayojua ni
Utakatifu ilhali wao hutenda yale yasiyo takatifu.
Wale wachungaji wanaojifanya kupenda na kuwajali kondoo, lakini
hawawajali tena, wataondolewa.
Msiwaguze wale WANGU walio na upako, pia msiwadhuru Manabii WANGU.
Msimpige mawe huyu mjumbe kwa kuwapa ujumbe WANGU. Kwa sababu madhara itamjia
yule atakayenena neno dhidi ya Mjumbe WANGU. Nijaribu MIMI na uone
Nakili haya na uwape wale wote walio na masikio ya kusikiliza. Wacha
wote wengine wabaki viziwi. Ingawa hawaamini, haimaanishi ya kwamba sitafanya
yale niliyoyazungumzia, itakuja kutendeka. Ezekiel 3:17-21 husema wape neno na
wasiposikiliza, damu haitakuwa mikononi mwako. Usipowapa onyo na kupitisha
unabii huu, basi watakufa katika dhambi
* * * * * * *
Ilipewa siku hii ya 12/31/96 kwake Rev. Sherrie Elijah kama hajaitarajia
alipokuwa anamwandikia mwingine kuwapa
www.allmightywind.com
www.almightywind.com
Contact AmightyWind